Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Baraka au Laana—Kuna Chaguo!
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Juni 15
    • 13. Kwa maneno yako mwenyewe, ungeelezaje baraka fulani ambazo Walawi walitamka?

      13 Sasa ebu wazia kwamba wasikia wale walio mbele ya Mlima Gerizimu wakiitikia kwa sauti kila baraka huku Walawi wakipaaza sauti hivi: “Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani. Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako. Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga. Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo.”—Kumbukumbu la Torati 28:3-6.

      14. Waisraeli wangepokea baraka kwa msingi upi?

      14 Msingi wa kupokea baraka hizi ulikuwa nini? Simulizi lasema hivi: “Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya BWANA, Mungu wako.” (Kumbukumbu la Torati 28:1, 2) Ndiyo, ufunguo wa kufurahia baraka za kimungu ulikuwa utii kwa Mungu. Lakini namna gani sisi leo? Je, sisi mmoja-mmoja tutachagua baraka na uhai kwa kuendelea ‘kusikiliza sauti ya Yehova’?—Kumbukumbu la Torati 30:19, 20, NW.

      Kuchunguza kwa Ukaribu Zaidi

      15. Ni jambo gani lililoonyeshwa katika baraka iliyorekodiwa kwenye Kumbukumbu la Torati 28:3, na twaweza kunufaikaje nalo?

      15 Acheni tufikirie baraka fulani ambazo Mwisraeli angeweza kufurahia kwa kumtii Yehova. Kwa kielelezo, Kumbukumbu la Torati 28:3 yasema: “Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.” Kubarikiwa na Mungu hakutegemei mahali wala mgawo. Huenda watu fulani wakahisi wamezuiwa katika hali zao, labda kwa sababu wanaishi katika eneo lililokumbwa na uharibifu wa mali za kimwili au katika nchi iliyogawanywa na vita. Huenda wengine wakatamani sana kumtumikia Yehova wakiwa kwingineko. Huenda wanaume fulani Wakristo wakavunjika moyo kwa sababu hawajawekwa rasmi kuwa watumishi wa huduma au kuwa wazee kutanikoni. Nyakati nyingine, wanawake Wakristo huhisi kufa moyo kwa sababu hawawezi kushiriki katika huduma ya wakati wote wakiwa mapainia au wamishonari. Hata hivyo, kila mtu ambaye ‘asikiliza sauti ya Yehova na kufanya kwa uangalifu yote anayotaka’ (NW) atabarikiwa sasa na kwa umilele wote.

      16. Kanuni ya Kumbukumbu la Torati 28:4 inaonwaje na tengenezo la Yehova leo?

      16 Kumbukumbu la Torati 28:4 yasema: “Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.” Matumizi ya kiwakilishi cha Kiebrania katika hali ya umoja kinachofasiriwa ‘-ako’ huonyesha kwamba hilo lingekuwa ono la kibinafsi la Mwisraeli mtiifu. Namna gani watumishi watiifu wa Yehova leo? Ongezeko na upanuzi wa ulimwenguni pote unaoendelea katika tengenezo la Mashahidi wa Yehova unatokana na baraka ya Mungu juu ya jitihada zenye bidii za wapiga-mbiu zaidi ya 5,000,000 wa habari njema za Ufalme. (Marko 13:10) Na uwezekano wa kuwa na ongezeko kubwa zaidi ni wazi kwa sababu watu zaidi ya 13,000,000 walihudhuria mwadhimisho wa Mlo wa Jioni wa Bwana wa 1995. Je, wewe unafurahia baraka za Ufalme?

      Chaguo la Israeli Lilileta Matokeo Tofauti

      17. ‘Kupatwa’ na baraka au laana kulitegemea nini?

      17 Kwa kweli, baraka zingemfuatia Mwisraeli mtiifu. Iliahidiwa hivi: “Baraka hizi zote zitakujilia na kukupata.” (Kumbukumbu la Torati 28:2) Vivyo hivyo, ilisemwa hivi juu ya laana: “Ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.” (Kumbukumbu la Torati 28:15) Ikiwa ungalikuwa Mwisraeli wa nyakati za kale, je, ‘ungalipatwa’ na baraka au na laana? Hilo lingalitegemea kama ulimtii Mungu au ulikosa kumtii.

  • Baraka au Laana—Kuna Chaguo!
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Juni 15
    • 19. Fafanua hali zilizofurahiwa wakati Yuda na Israeli yalipochagua kumtii Yehova.

      19 Baraka zilikuwa nyingi na utulivu ulienea wakati tu ambapo Israeli walimtii Yehova. Kwa kielelezo, kuhusu siku za Mfalme Sulemani, twasoma hivi: “Yuda na Israeli walikuwa wengi kama mchanga wa pwani kwa wingi, wakila, na kunywa, na kufurahi. . . . Yuda na Israeli wakakaa salama, kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, tokea Dani mpaka Beer-sheba, siku zote za Sulemani.” (1 Wafalme 4:20-25) Hata wakati wa Mfalme Daudi, uliokuwa wenye upinzani mwingi kutoka kwa maadui wa Mungu, taifa lilihisi utegemezo na baraka ya Yehova wakati lilipochagua kumtii Mungu wa ukweli.—2 Samuel 7:28, 29; 8:1-15.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki