Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 19. Jamii ya Yohana ilishughulikiaje madaraka ambayo ilipewa na Yesu katika 1919, kukiwa na tokeo gani?

      19 Tangu 1919 na kuendelea mabaki ya wapakwa-mafuta, wakifuata kielelezo cha Yesu, walianzisha kampeni yenye bidii ya kutangaza kotekote habari njema za Ufalme. (Mathayo 4:17; Warumi 10:18) Kama tokeo, wengine wa lile sinagogi la Shetani la ki-siku-hizi, Jumuiya ya Wakristo, walijia baki hili la wapakwa-mafuta, wakatubu na ‘wakainama,’ wakikiri mamlaka ya mtumwa huyo. Wao vilevile walikuja kutumikia Yehova katika muungano na wale wazee-wazee wa jamii ya Yohana. Hilo liliendelea mpaka hesabu kamili ya ndugu wapakwa-mafuta wa Yesu wakakusanywa.

  • “Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • [Picha katika ukurasa wa 63]

      Kusaidia Wengi Wainame Chini

      Kati ya wale wapakwa-mafuta 144,000 ambao watarithi Ufalme wa kimbingu, inaonekana kwamba baki, ile jamii ya Yohana, ya walio punde kuliko 9,000 wangali watamaliza mwendo wao duniani. Wakati ule ule, umati mkubwa umepanuka ukawa 6,600,000 na zaidi. (Ufunuo 7:4, 9) Ni kitu gani kimesaidia kutokeza ongezeko hili kubwa mno? Zile shule mbalimbali zinazoongozwa na Mashahidi wa Yehova zimetoa mchango mkubwa. Tofauti sana na seminari za Jumuiya ya Wakristo ambazo hufundisha falsafa za kilimwengu na kushusha heshima ya Biblia, shule hizi za Mashahidi hukaza kikiki imani yenye kina katika Neno la Mungu. Zinaonyesha utumizi walo wenye mafaa kwa habari ya maisha safi ya adili na utumishi ulio wakfu kwa Mungu. Ulimwenguni pote tangu 1943, kila kundi la Mashahidi wa Yehova huongoza Shule ya Huduma ya Kitheokrasi katika Jumba la Ufalme lalo la mahali pao. Mamilioni huhudhuria shule hii kila juma, wakifuata programu yenye umoja ya elimu ya Biblia.

      Tangu 1959 Mashahidi wa Yehova wameongoza pia Shule za Huduma ya Ufalme kwa ajili ya kuzoeza wazee na watumishi wa huduma wa kundi. Na tangu 1977, ile Shule ya Utumishi wa Painia imezoeza mamia ya maelfu ya akina ndugu na dada ambao, wakiwa na roho ya kweli ya Kifiladelfia, wanatumikia Yehova wakati wote katika kazi ya kuhubiri. Katika 1987 ile Shule ya Mazoezi ya Kihuduma ilianzishwa kwa ajili ya kuzoeza Mashahidi wa kiume kwa ajili ya migawo ya pekee katika shamba la ulimwengu.

      Yenye kutokeza miongoni mwa shule zinazoendeshwa na Mashahidi wa Yehova imekuwa ile Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi. Tangu 1943 shule hii ya misionari, iliyoko Mkoa wa New York imehitimisha vikundi viwili vya wanafunzi karibu kila mwaka. Kwa ujumla, imezoeza wahudumu wa Yehova zaidi ya 7,000 kwa ajili ya utumishi wa misionari wa nchi za kigeni. Wahitimu wa shule hii wametumikia katika mabara zaidi ya 100, katika mengi yayo walisaidia sana katika kufungua kazi ya Ufalme. Baada ya miaka yapata 60, wengi wa wale wamisionari wa mapema wangali kazini, wakishiriki pamoja na wamisionari wapya zaidi katika kusogeza mbele katika tufe lote mpanuko wa tengenezo la Yehova. Lo! huo umekuwa mpanuko mzuri ajabu kama nini!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki