-
Wana-Farasi Wanne Katika Mwendo!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
23. Ni nini kinachodokezwa na taarifa, “Usidhuru mafuta ya zeituni na divai”?
23 Ni nini kinachodokezwa na taarifa, “Usidhuru mafuta ya zeituni na divai”? Wengine wameiona kuwa ikimaanisha kwamba ingawa wengi wangepungukiwa na chakula na hata wafe njaa, vitu vya anasa vya matajiri havingedhuriwa. Lakini katika Mashariki ya Kati, mafuta na divai si vitu vya anasa kwa kweli. Katika nyakati za Biblia, mkate, mafuta, na divai vilionwa kuwa chakula kikuu. (Linga Mwanzo 14:18; Zaburi 104:14, 15.) Sikuzote maji hayakuwa safi, kwa hiyo divai ilitumiwa sana kwa kunywa na nyakati nyingine kwa makusudi ya kitiba. (1 Timotheo 5:23) Kwa habari ya mafuta, katika siku ya Eliya mjane wa Sarepta, ajapokuwa maskini, bado alikuwa amebakiza mafuta kiasi fulani ya kupikia unga wake uliobaki. (1 Wafalme 17:12) Kwa hiyo, amri “usidhuru mafuta ya zeituni na divai” inaonekana kuwa shauri la kutotumia bidhaa hizo za msingi kwa uharaka mno lakini kuzitumia kwa kulimbika. La sivyo, ‘zitadhuriwa,’ yaani, zitakwisha kabla ya njaa kwisha.
-
-
Wana-Farasi Wanne Katika Mwendo!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
na usidhuru mafuta ya zeituni na divai.’” (Ufunuo 6:6, NW)
-