Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Lo! Jinsi Kilivyo Kina cha Hekima ya Mungu!’
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Mei 15
    • 17. Jambo ambalo Yehova alifanya lilikuwa “kinyume cha asili” jinsi gani?

      17 Yehova alifanya jambo ambalo wengi hawakutazamia kabisa. Paulo anaeleza yale yaliyotukia kuwa “kinyume cha asili.” (Rom. 11:24) Hilo lilitukia jinsi gani? Kwa kweli, lingeonekana kuwa jambo lisilo la kawaida, hata lisilo la asili, kupandikiza tawi la mwituni kwenye mti uliopandwa, lakini hivyo ndivyo wakulima fulani walivyofanya katika karne ya kwanza.b Kwa njia hiyohiyo, Yehova alifanya jambo fulani lisilo la kawaida. Kwa maoni ya Wayahudi, Watu wa Mataifa hawangeweza kuzaa matunda yenye kukubalika. Hata hivyo, Yehova aliwafanya watu hao wa mataifa kuwa sehemu ya “taifa” ambalo lilizaa matunda ya Ufalme. (Mt. 21:43)

  • ‘Lo! Jinsi Kilivyo Kina cha Hekima ya Mungu!’
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Mei 15
    • a Bila shaka, hakuna mzeituni ambao unafananisha kikundi fulani halisi cha watu au kikundi cha mfano. Ingawa Waisraeli wa asili walitokeza wafalme na makuhani, taifa hilo halikuwa ufalme wa makuhani. Wafalme katika Israeli walikatazwa na sheria wasiwe makuhani. Kwa hiyo, Waisraeli wa asili hawakutumika wakiwa mzeituni halisi. Paulo anaonyesha jinsi kusudi la Mungu la kutokeza “ufalme wa makuhani” linavyotimizwa kuhusiana na Israeli wa kiroho. Habari hii inarekebisha maelezo yaliyochapishwa katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 15, 1984, ukurasa wa 7-12.

  • ‘Lo! Jinsi Kilivyo Kina cha Hekima ya Mungu!’
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Mei 15
    • [Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 24]

      Kwa Nini Matawi ya Mzeituni wa Mwituni Yalipandikizwa?

      ▪ Lucius Junius Moderatus Columella alikuwa askari-jeshi Mroma na mkulima aliyeishi katika karne ya kwanza W.K. Anajulikana sana kwa sababu ya vitabu 12 alivyoandika kuhusu maisha ya mashambani na ukulima.

      Katika kitabu chake cha tano, anataja methali hii ya zamani: “Anayelima shamba la mizeituni, analiomba matunda; anayelitilia mbolea, analisihi limpe matunda; na yule anayekata matawi yake, analilazimisha lizae matunda.”

      Baada ya kueleza kuhusu miti inayositawi na bado haizai matunda, anapendekeza utaratibu ufuatao: “Ni mpango mzuri kutoboa miti hiyo kwa kifaa kama vile msumari na kuingiza ndani kabisa ya shimo hilo tawi dogo la kijani kibichi lililochukuliwa kutoka kwenye mzeituni wa mwituni; matokeo ni kwamba mti huo, kwa kuwa umetiwa au kupachikwa mche wenye kuzaa, unazaa zaidi.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki