Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Lo! Jinsi Kilivyo Kina cha Hekima ya Mungu!’
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Mei 15
    • 15 Basi, Yehova alifanya nini ili kutimiza kusudi lake? Paulo anaeleza kwamba matawi kutoka kwenye mzeituni wa mwituni yalipandikizwa kwenye mzeituni uliopandwa ili kuchukua mahali pa yale matawi yaliyokatwa. (Soma Waroma 11:17, 18.) Hivyo, Wakristo watiwa-mafuta wa mataifa, kama Wakristo fulani katika kutaniko la Roma, walipandikizwa kwa njia ya mfano kwenye mzeituni huo wa mfano. Katika njia hiyo walikuja kuwa sehemu ya uzao wa Abrahamu. Mwanzoni, walikuwa kama matawi ya mzeituni wa mwituni, kwa sababu hawakuwa na nafasi yoyote ya kuwa sehemu ya agano hilo la pekee. Lakini Yehova aliwafungulia njia ili wawe Wayahudi wa kiroho.—Rom. 2:28, 29.

  • ‘Lo! Jinsi Kilivyo Kina cha Hekima ya Mungu!’
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Mei 15
    • 17. Jambo ambalo Yehova alifanya lilikuwa “kinyume cha asili” jinsi gani?

      17 Yehova alifanya jambo ambalo wengi hawakutazamia kabisa. Paulo anaeleza yale yaliyotukia kuwa “kinyume cha asili.” (Rom. 11:24) Hilo lilitukia jinsi gani? Kwa kweli, lingeonekana kuwa jambo lisilo la kawaida, hata lisilo la asili, kupandikiza tawi la mwituni kwenye mti uliopandwa, lakini hivyo ndivyo wakulima fulani walivyofanya katika karne ya kwanza.b Kwa njia hiyohiyo, Yehova alifanya jambo fulani lisilo la kawaida. Kwa maoni ya Wayahudi, Watu wa Mataifa hawangeweza kuzaa matunda yenye kukubalika. Hata hivyo, Yehova aliwafanya watu hao wa mataifa kuwa sehemu ya “taifa” ambalo lilizaa matunda ya Ufalme. (Mt. 21:43) Kuanzia mwaka wa 36 W.K., wakati Kornelio, Mtu wa kwanza wa Mataifa asiyetahiriwa alipogeuzwa imani na kutiwa mafuta, mlango ulifunguliwa kwa watu wasio Wayahudi ambao hawakuwa wametahiriwa kupandikizwa kwenye mzeituni huo wa mfano.—Mdo. 10:44-48.c

      18. Wayahudi wa asili walikuwa na nafasi gani baada ya mwaka wa 36 W.K.?

      18 Je, hilo linamaanisha kwamba baada ya mwaka wa 36 W.K., Wayahudi wa asili hawakuwa tena na nafasi ya kuwa sehemu ya uzao wa Abrahamu? Hapana. Paulo anaeleza: “Wao pia [Wayahudi wa asili], ikiwa hawatadumu katika ukosefu wao wa imani, watapandikizwa; kwa maana Mungu anaweza kuwapandikiza tena. Kwa maana ikiwa wewe ulikatwa kutoka kwenye mzeituni ulio wa asili ya mwituni na kupandikizwa kinyume cha asili katika mzeituni wa bustanini, si afadhali zaidi kwamba hawa walio wa asili wapandikizwe katika mzeituni wao wenyewe!”d—Rom. 11:23, 24.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki