-
Watazame Mayatima na Wajane Katika Dhiki YaoMnara wa Mlinzi—2001 | Juni 15
-
-
Pedro hamkumbuki mama yake aliyekufa alipokuwa na umri wa mwaka mmoja na nusu. Alipokuwa na umri wa miaka mitano babake pia akafa. Kwa hiyo Pedro na ndugu zake waliachwa bila wazazi. Mashahidi wa Yehova walikuwa wamemtembelea baba yao, kwa hiyo Pedro na ndugu zake wote wakubwa walianza kujifunza Biblia.
Pedro asimulia: “Juma lililofuata, tulianza kuhudhuria mikutano. Tuliposhirikiana na ndugu, tuliweza kuona jinsi walivyotupenda. Kutaniko lilikuwa kimbilio langu kwa kuwa ndugu na dada walinipenda kana kwamba walikuwa wazazi wangu.” Pedro anakumbuka kwamba mzee mmoja Mkristo alikuwa akimkaribisha nyumbani kwake, na aliweza kushiriki mazungumzo na burudisho pamoja na familia ya mzee huyo. “Nakumbuka pindi hizo na ninazithamini sana,” Pedro anasema. Pedro alianza kuhubiri juu ya imani yake alipokuwa na umri wa miaka 11, na kubatizwa alipokuwa na umri wa miaka 15. Ndugu zake wakubwa pia walisaidiwa na ndugu kutanikoni kufanya maendeleo makubwa ya kiroho.
David ni mfano mwingine. David na dada yake, ambao ni mapacha, waliachwa peke yao wazazi wao walipotengana. Walilelewa na babu na nyanya zao na dada mmoja ya mama yao. “Tulipokua na kutambua hali yetu, tulipatwa na wasiwasi na huzuni nyingi sana. Tulihitaji tegemezo. Dada huyo wa mama yangu akawa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, kwa hiyo tukafundishwa kweli ya Biblia. Ndugu walituonyesha upendo na urafiki. Walitupenda sana, na kututia moyo kufikia miradi na kuendelea kumtumikia Yehova. Nilipokuwa na umri wa miaka kumi hivi, mtumishi wa huduma mmoja alikuwa akija kunichukua tuhubiri pamoja. Ndugu mwingine alinisaidia kifedha nilipohudhuria mikusanyiko. Ndugu mmoja hata alinipa fedha niweze kutoa michango kwenye Jumba la Ufalme.”
David alibatizwa alipokuwa na umri wa miaka 17, na baadaye akaanza kutumikia kwenye ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova huko Mexico. Anasema hivi: “[Hata sasa] kuna wazee kadhaa ambao wananielimisha na kunitolea ushauri unaonisaidia. Kwa njia hiyo ninaweza kushinda wasiwasi na upweke.”
-
-
Watazame Mayatima na Wajane Katika Dhiki YaoMnara wa Mlinzi—2001 | Juni 15
-
-
Mzee mwingine wa kutaniko ambaye amezoea kuwasaidia mayatima na wajane anasema hivi: “Ninaamini kwamba mayatima wana uhitaji mkubwa zaidi wa upendo wa Kikristo kuliko hata wajane. Nimeona kwamba mayatima wengi wanahisi wamepuuzwa kuliko watoto na vijana walio na wazazi wawili. Wanahitaji kuonyeshwa upendo mara nyingi. Ni vyema kuwatafuta baada ya mikutano na kuwajulia hali. Kuna ndugu aliyeoa ambaye alipoteza wazazi alipokuwa mvulana mdogo. Huwa ninamsalimu kwa uchangamfu mikutanoni, na yeye hunikumbatia anaponiona. Jambo hilo huimarisha upendo wa kidugu.”
-