-
“Mungu wa Pekee wa Kweli” Ni Nani?Amkeni!—2005 | Aprili 22
-
-
Chanzo cha Utatu
Biblia inataja kwamba kuna miungu mingi inayoabudiwa na watu, kutia ndani Ashtorethi, Milkomu, Kemoshi, na Moleki. (1 Wafalme 11:1, 2, 5, 7) Hata watu wengi katika taifa la kale la Israeli wakati mmoja waliamini kwamba Baali ndiye Mungu wa kweli. Kwa hiyo, Eliya, nabii wa Yehova akawaambia hivi: “Ikiwa Yehova ndiye Mungu wa kweli, mfuateni yeye; lakini ikiwa ni Baali, mfuateni yeye.”—1 Wafalme 18:21.
Kabla ya Yesu kuzaliwa, wapagani walizoea kuabudu miungu mitatu-mitatu. Mwanahistoria Will Durant anasema: “Dhana za utatu mtakatifu zilianzia Misri.” Katika kichapo kimoja (Encyclopædia of Religion and Ethics) James Hastings aliandika: “Kwa mfano, katika dini ya Kihindi kuna miungu watatu: Brahmā, Siva, na Viṣṇu; na katika dini ya Misri kuna miungu watatu Osiris, Isis, na Horus.”
-
-
“Mungu wa Pekee wa Kweli” Ni Nani?Amkeni!—2005 | Aprili 22
-
-
[Picha katika ukurasa wa 7]
MISRI
Utatu wa Horus, Osiris, na Isis, katika milenia ya pili K.W.K.
[Picha katika ukurasa wa 7]
PALMYRA, SYRIA
Utatu wa mungu mwezi, Bwana wa Mbingu, na mungu jua, karne ya kwanza hivi W.K.
[Picha katika ukurasa wa 7]
INDIA
Utatu wa mungu wa Kihindu, karne ya saba hivi W.K.
-