-
Papua New Guinea2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Alipokuwa akitoa hotuba mbele ya kutaniko au kikundi cha mbali, John aliandika jina lake na la mtafsiri kwenye ubao mweusi. Kisha, akaelekeza kidole mbinguni, na kuwauliza wasikilizaji, “Mungu, jina lake nani?” Akaandika jibu lao, “Yehova” na “Zaburi 83:18” juu ya ubao huo. Chini yake upande wa kushoto, aliandika kichwa “Ulimwengu wa Kale” na kuchora wanaume wawili wakipigana, mtu akilia, kaburi, na “Waroma 5:12.” Upande wa kulia, akaandika kichwa “Ulimwengu Mpya” na kuchora wanaume wawili wakisalimiana kwa mikono, mtu akitabasamu, kaburi lililofutwa, na “Ufunuo 21:4.” Baadaye, alitoa hotuba yenye kusisimua ili kueleza michoro yake. Kisha akawakaribisha wasikilizaji wasimame mbele na kurudia hotuba yake. Walipokuwa wameelewa, aliwaambia wachore picha hizo kwenye karatasi na kuzitumia katika kazi ya kuhubiri.
Mahubiri hayo yaliyokuja kuitwa “Mahubiri ya Kwanza ya Picha” yalikuwa na matokeo makubwa sana katika kazi ya kuhubiri nchini Papua New Guinea. Mahubiri mengine ya picha yalifuata. “Tulitumia saa nyingi kunakili picha hizo za mahubiri kwenye vitabu vya kuandikia shuleni. Kila mwanafunzi wa Biblia alipata nakala ambayo alitumia kuwafundisha wengine,” anasema Lena Davison aliyetumika katika nchi hiyo kwa miaka 47. Watoto walichora picha kwenye vitabu vyao na wakafurahia sana kuvipaka rangi.
Mbinu hiyo ya kufundisha ilitumiwa pia katika mikutano ya kutaniko. “Michoro kwenye ubao ilitumiwa sana wakati wa Mikutano ya Watu Wote na Funzo la Mnara wa Mlinzi, na hilo likawasaidia sana wale ambao hawakujua kusoma,” anaeleza Joyce Willis, painia kutoka Kanada aliyekaa zaidi ya miaka 40 nchini Papua New Guinea. Mahubiri ya picha yaliyochorwa juu ya turubai yalitumiwa pia katika makusanyiko. “Picha hizo kubwa zilipendwa sana na zilikazia mafundisho muhimu katika akili za wasikilizaji,” anasema Mike Fisher aliyekuwa mwangalizi wa mzunguko huko. “Picha nyingi kati ya hizo ziliishia katika nyumba za wahubiri waliokuwa katika maeneo ya mbali, ambao walizitumia kuwahubiria wageni.”
Miaka mingi baadaye, watu wengi zaidi walipojifunza kusoma na kuandika na vichapo vyenye picha vikapatikana kwa wingi, mahubiri ya picha yakaacha kutumiwa.
-
-
Papua New Guinea2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 89]
Hotuba ya picha
-