-
Suluhisho la Tatizo la Ulimwenguni PoteMnara wa Mlinzi—2009 | Desemba 1
-
-
Mambo Ambayo Ufalme wa Mungu Utafanya
Mungu atatimiza ahadi zake kupitia mtu wa pili aliye na nguvu ulimwenguni, yaani, Yesu Kristo aliyefufuliwa. Karibuni, Yesu atatawala bila kupingwa akiwa Mfalme juu ya dunia yote. Wanadamu hawatatawaliwa tena na wafalme, marais, au wanasiasa. Badala yake, watatawaliwa na Mfalme mmoja na serikali moja, yaani, Ufalme wa Mungu.
Ufalme huo utaharibu serikali zote za kibinadamu. Biblia ilitabiri hivi zamani za kale: “Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote, nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo.” (Danieli 2:44) Watu kutoka sehemu zote za dunia wataunganishwa chini ya serikali moja yenye uadilifu, yaani, Ufalme wa Mungu.
Alipokuwa mwanadamu hapa duniani, Yesu alizungumza mara nyingi kuhusu Ufalme huo. Aliutaja katika ile sala ya kielelezo, alipowaagiza wanafunzi wake wasali hivi: “Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.” (Mathayo 6:10) Ona kwamba Yesu alionyesha Ufalme huo unahusianishwa na kutendeka kwa mapenzi ya Mungu duniani, na kwamba ni mapenzi ya Mungu kuondoa kuteseka duniani pote.
Serikali adilifu ya Mungu italeta baraka ambazo hakuna serikali yoyote ya kibinadamu inaweza kuleta. Kumbuka kwamba Mungu alimtoa Mwana wake awe fidia ili wanadamu waweze kuishi milele. Chini ya Mtawala mwenye ukarimu wa Ufalme huo, watu watafikia ukamilifu hatua kwa hatua. Matokeo yatakuwa nini? Yehova “kwa kweli atameza kifo milele, na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hakika atafuta machozi katika nyuso zote.”—Isaya 25:8.
-
-
Suluhisho la Tatizo la Ulimwenguni PoteMnara wa Mlinzi—2009 | Desemba 1
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 7]
Maandiko Yanayoonyesha Wakati Ujao Mzuri
HAKUTAKUWA NA VITA TENA:
“Njooni, tazameni matendo ya Yehova, jinsi ambavyo ameweka matukio ya kushangaza duniani. Anakomesha vita mpaka kwenye mwisho wa dunia.”—Zaburi 46:8, 9.
WAPENDWA WALIOKUFA WATARUDI:
“Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.”—Matendo 24:15.
KILA MTU ATAKUWA NA CHAKULA:
“Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani; juu ya milima kutakuwa na mafuriko.”—Zaburi 72:16.
HAKUTAKUWA TENA NA MAGONJWA:
“Hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’”—Isaya 33:24.
WATU WAOVU WATAONDOLEWA:
“Nao waovu, watakatiliwa mbali kutoka duniani; nao wenye hila, watang’olewa kutoka ndani yake.”—Methali 2:22.
KUTAKUWA NA HAKI:
“Tazama! Mfalme [Kristo Yesu] atatawala kwa ajili ya uadilifu; nao wakuu watatawala wakiwa wakuu kwa ajili ya haki.”—Isaya 32:1.
-