-
Nanga Yao Ni Tumaini, Nao Huchochewa na UpendoMnara wa Mlinzi—1999 | Julai 15
-
-
9. Wakristo fulani wachache waliojiweka wakfu wanafanya nini, na mambo hayo yapaswa kutufanya tufikirie nini?
9 Yaonekana kwamba Wakristo fulani wachache waliojiweka wakfu katika sehemu kadhaa za ulimwengu wamekunja matanga ya meli yao ya imani. Meli ingali yaelea, lakini badala ya kusonga mbele katika imani kamili, wao wameamua kwenda polepole. Wengine waliovutiwa na tumaini la “Paradiso ya hivi karibuni” walikuwa tayari kujitahidi ili kuifikia—walikuwa na bidii katika kazi ya kuhubiri nao walihudhuria kwa ukawaida mikutano, makusanyiko na mikusanyiko yote. Lakini sasa wanafikiri kwamba utimizo wa matumaini yao uko mbali kuliko walivyotazamia, nao wamepunguza bidii yao. Jambo hilo laonekana waziwazi kupitia utendaji wa kuhubiri uliopunguka, kutohudhuria mikutano kwa ukawaida, na kuwa tayari kukosa sehemu kadhaa za programu ya makusanyiko au ya mikusanyiko. Wengine wanatumia wakati mwingi zaidi katika tafrija na kutafuta starehe za mali. Mambo hayo hutufanya tufikirie kile kipasacho kuwa kichocheo maishani mwetu kupatana na wakfu wetu kwa Yehova. Je, bidii yetu katika utumishi wake yapasa itegemee lile tumaini la “Paradiso ya hivi karibuni”?
-
-
Nanga Yao Ni Tumaini, Nao Huchochewa na UpendoMnara wa Mlinzi—1999 | Julai 15
-
-
Kuchochewa na Upendo na Roho Takatifu
13, 14. (a) Kwa nini nanga ya tumaini letu pekee haitoshi? (b) Ni kani gani ipasayo kutuchochea tumtolee Yehova utumishi mtakatifu, na kwa nini?
13 Mkristo hatasonga mbele kuelekea mfumo mpya ikiwa nia pekee inayomfanya amtumikie Yehova ni lile tumaini la kuishi milele katika dunia paradiso. Huku akihifadhi nanga yake ya tumaini ikiwa jambo la kuyaweka thabiti maisha yake, yeye ahitaji kuiongezea imani yake kani inayochochea ya upendo. Paulo alikazia jambo hilo alipoandika hivi: “Kwabaki imani, tumaini, upendo, matatu haya; lakini lililo kubwa zaidi sana kati ya haya ni upendo.”—1 Wakorintho 13:13.
14 Kani inayotuchochea kumtolea Yehova utumishi mtakatifu yapasa kuwa upendo wenye kuhisiwa moyoni kwa Yehova, kwa kuitikia upendo wake usio na kipimo kwetu. Mtume Yohana aliandika hivi: “Yeye ambaye hapendi hajaja kujua Mungu, kwa sababu Mungu ni upendo. Kwa hili upendo wa Mungu ulifanywa dhahiri katika kisa chetu, kwa sababu Mungu alituma Mwana wake mzaliwa-pekee kuingia katika ulimwengu ili tuweze kupata uhai kupitia kwake. Kwa habari yetu, twapenda, kwa sababu yeye alitupenda sisi kwanza.” (1 Yohana 4:8, 9, 19) Kwa sababu ya shukrani zetu kwa Yehova, hangaiko letu kuu lapaswa kuwa kushuhudia utakaso wa jina lake takatifu na utetezi wa enzi kuu yake yenye uadilifu, wala si kupata wokovu wa kibinafsi.
15. Upendo wetu kwa Yehova unahusianaje na suala la enzi kuu yake?
15 Yehova ataka tumtumikie kwa sababu twampenda yeye, wala si Paradiso tu. Ensaiklopedia ya Biblia Insight on the Scriptures,a yataarifu hivi: “Yehova hufurahia jambo la kwamba enzi kuu yake na jinsi viumbe wake waitegemezavyo hutegemea upendo hasa. Yeye huwapenda tu wale wanaoipenda enzi kuu yake kwa sababu ya sifa zake bora na kwa sababu hiyo ni adilifu, wanaoipendelea enzi kuu yake kuliko nyingine yoyote. (1 Ko 2:9) Wao huchagua kutumikia chini ya enzi kuu yake badala ya kujaribu kujitegemea—hiyo ni kwa sababu ya ujuzi wao kumhusu yeye na upendo wake, haki yake, na hekima yake, ambazo wao hutambua zinazidi sana zao. (Zab 84:10, 11)”—Buku la 2, ukurasa wa 275.
-