Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Bustani Nzuri
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
    • Wanyama, maua, miti, na maji yanayotiririka katika bustani nzuri ya Edeni

      HADITHI YA 2

      Bustani Nzuri

      TAZAMA dunia hii! Kila kitu ni kizuri sana! Tazama majani na miti, maua na wanyama wote. Unaweza kumjua tembo na simba hapa?

      Bustani hii nzuri ilitokea namna gani? Na tuone Mungu alivyotuwekea dunia tayari.

      Kwanza, Mungu aliumba majani mabichi yaifunike nchi. Alifanya namna zote za mimea na miti midogo. Mimea hiyo inapamba dunia. Zaidi ya hivyo, mimea mingi inatupa chakula kitamu sana.

      Tena Mungu aliumba samaki waogelee katika maji na ndege waruke katika anga. Aliumba mbwa na paka na farasi; wanyama wakubwa na wadogo. Ni wanyama gani wanaokaa karibu na nyumba yenu? Je! si vizuri kufurahi kwa vile Mungu alitufanyia vyote hivyo?

      Halafu, Mungu alifanya sehemu moja ya dunia kuwa ya pekee sana. Aliita bustani ya Edeni. Ilikuwa nzuri sana. Kila kitu ndani kilikuwa kizuri. Mungu alitaka dunia nzima iwe kama bustani nzuri hii.

      Lakini tazama tena picha hii ya bustani. Je! unajua kitu ambacho Mungu aliona hakipo? Tuone.

      Mwanzo 1:11-25; 2:8, 9.

  • Mwanamume na Mwanamke wa Kwanza
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
    • Adamu na Hawa wakiwa katika bustani ya Edeni

      HADITHI YA 3

      Mwanamume na Mwanamke wa Kwanza

      UNAONA tofauti gani katika picha hii? Kuna watu. Mwanamume na mwanamke wa kwanza. Nani aliwaumba? Ni Mungu. Unajua jina lake? Ni Yehova. Mwanamume na mwanamke waliitwa Adamu na Hawa.

      Yehova Mungu aliumba Adamu hivi. Alichukua mavumbi akafanya mwili mzuri wa mwanamume. Kisha akapuliza katika pua, Adamu akawa hai.

      Yehova Mungu alimpa Adamu kazi ya kuwapa wanyama wote majina. Labda Adamu aliwatazama wanyama muda mrefu ili aweze kuwachagulia wote majina bora. Adamu alipokuwa akiwapa wanyama majina, aliona jambo fulani. Unajua ni jambo gani?

      Wanyama wote walikuwa na wenzao. Tembo baba na mama walikuwapo, hata simba baba na mama. Lakini Adamu hakuwa na mwenzake. Basi Yehova akampa Adamu usingizi mzito, akachukua ubavu wake mmoja. Kwa ubavu huo, Yehova alimfanyia Adamu mke.

      Adamu akafurahi! Wazia Hawa alivyofurahi alipowekwa katika bustani hiyo nzuri! Wangeweza kuzaa watoto wakae pamoja kwa furaha.

      Yehova alitaka Adamu na Hawa wakae milele. Alitaka waifanye dunia nzima iwe nzuri kama bustani hii ya Edeni. Adamu na Hawa walifurahia sana hilo! Wewe ungependa kuifanya dunia iwe bustani nzuri? Lakini furaha ya Adamu na Hawa haikuendelea. Na tuone kwa nini.

      Zaburi 83:18; Mwanzo 1:26-31; 2:7-25.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki