Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Alinifundisha Kufanya Mapenzi Yake
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 15
    • Darasa letu la Gileadi lilikuwa na wanafunzi 120 kutoka kila pembe ya dunia. Hatukuambiwa kuhusu migawo yetu mpaka siku ya kuhitimu ilipofika. Tulienda haraka katika maktaba ya Gileadi ili kujifunza kuhusu nchi ambako tulitumwa. Niligundua kwamba nchi ya Paraguai, ambako nilitumwa, ilikuwa na historia ya mapinduzi ya kisiasa. Muda mfupi baada ya kufika huko, niliwauliza asubuhi moja wamishonari wengine kulikuwa na “sherehe” gani wakati wa usiku. Walitabasamu na kusema: “Umeshuhudia mapinduzi yako ya kwanza. Tazama nje upande wa mbele.” Wanajeshi walikuwa kila mahali!

      KUKABILI HALI YA HATARI

      Pindi moja, nilienda pamoja na mwangalizi wa mzunguko alipotembelea kutaniko la mashambani ili kuonyesha sinema ya The New World Society in Action. Tulisafiri kwa saa nane au tisa, kwanza kwa gari-moshi, kisha kwa farasi na gari la kukokotwa na farasi, na hatimaye gari linalokokotwa na ng’ombe. Tulibeba jenereta na mashini ya kuonyesha sinema. Mwishowe, baada ya kufika mahali tulipokuwa tukienda, siku iliyofuata tulitembelea eneo lenye mashamba na kuwaalika wote waje kuona sinema hiyo usiku huo. Watu 15 walihudhuria.

      Baada ya kuonyesha sinema hiyo kwa dakika 20, tuliambiwa tuingie ndani ya nyumba haraka iwezekanavyo. Tulichukua haraka mashini ya kuonyesha sinema na tukatii. Huo ndio wakati ambapo wanaume fulani walianza kupiga kelele, kufyatua risasi, na kupaaza sauti hivi: “Mungu wetu ni mungu mwenye kiu ya damu, naye anataka damu ya gringos.” Kulikuwa tu na gringos au wageni wawili hapo, na mimi nilikuwa mmoja wao! Wale waliokuja kuona sinema hiyo waliuzuia umati huo uliojaribu kuvunja nyumba na kuingia ndani. Lakini wapinzani hao walirudi karibu saa tisa usiku, wakifyatua risasi na kuapa kwamba wangeturudisha mjini siku hiyo.

      Akina ndugu walimjulisha mkuu wa polisi, ambaye alikuja alasiri na farasi wawili ili aturudishe mjini. Tulipokuwa njiani, kila mara tulipofika mahali penye vichaka au miti, mkuu huyo wa polisi alitoa bunduki yake na kwenda mbele ili akague eneo hilo. Niliona kwamba farasi walikuwa njia muhimu ya usafiri, kwa hiyo baadaye nilinunua farasi mmoja.

      WAMISHONARI ZAIDI WANAFIKA

      Kazi ya kuhubiri iliendelea kufanikiwa licha ya upinzani wa mara kwa mara wa makasisi. Katika mwaka wa 1955, wamishonari wapya watano walifika, kutia ndani dada kijana kutoka Kanada aliyeitwa Elsie Swanson, ambaye alihitimu katika darasa la 25 la Gileadi. Tulikuwa pamoja kwa kipindi fulani kwenye ofisi ya tawi kabla hajapewa mgawo katika mji mwingine. Alikuwa ametumia maisha yake yote katika utumishi wa Yehova kwa msaada mdogo kutoka kwa wazazi wake, ambao hawakuwahi kamwe kukubali kweli. Mnamo Desemba 31, 1957, mimi na Elsie tulifunga ndoa, na tuliishi peke yetu katika nyumba ya wamishonari kusini mwa Paraguai.

      Nyumba yetu haikuwa na maji ya bomba; badala yake, tulikuwa na kisima nyuma ya nyumba. Kwa hiyo, hakukuwa na bafu au choo ndani ya nyumba, wala mashini ya kufua, au hata friji. Tulinunua vyakula vya kupika kila siku. Lakini kuwa na maisha rahisi na mahusiano yenye upendo pamoja na ndugu na dada zetu kutanikoni kulifanya kipindi hicho kiwe kipindi chenye furaha sana katika maisha yetu ya ndoa.

  • Yehova Alinifundisha Kufanya Mapenzi Yake
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 15
    • [Picha katika ukurasa wa 20]

      Siku yetu ya arusi, Desemba 31, 1957

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki