Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu?
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Septemba 1
    • Jambo tunalopaswa kufikiria ni ikiwa kiumbe mkamilifu aliyeumbwa na Mungu angeweza kufanya mambo yasiyo sawa. Badala ya kuwaumba viumbe wake kama mashine, Mungu aliwapa uhuru wa kuchagua, yaani, uwezo wa kufanya maamuzi yao wenyewe. Hivyo, kiumbe mkamilifu mwenye akili anaweza kuchagua kutenda mema au mabaya. Kwa kweli, mambo yanayofanywa tu na kiumbe mwenye akili, awe mwanadamu au kiumbe wa roho aliyepewa uhuru wa kuchagua, ndiyo yanayoweza kuwa makosa au sawa kimaadili.

      Kwa hiyo, Mungu hangewapa viumbe wake uhuru wa kuchagua na wakati huohuo awazuie kufanya mabaya ikiwa wangeamua kufanya hivyo. Yesu alizungumzia kuhusu matumizi mabaya ya uhuru wa kuchagua aliposema hivi kumhusu Ibilisi: “Hakusimama imara katika kweli.” (Yohana 8:44) Maneno hayo yanaonyesha waziwazi kwamba kiumbe wa roho ambaye mwanzoni alikuwa mkamilifu, alikuja kuwa Ibilisi, ingawa wakati fulani ‘alisimama imara katika kweli.’a Yehova Mungu aliwaumba viumbe wake wakiwa na uhuru wa kuchagua kwa sababu anawapenda na kuwaamini.—Ona sanduku “Je, Kiumbe Mkamilifu Angeweza Kupoteza Ukamilifu?” kwenye ukurasa wa 6.

  • Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu?
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Septemba 1
    • [Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 6]

      Je, Kiumbe Mkamilifu Angeweza Kupoteza Ukamilifu?

      Ukamilifu ambao Mungu amewapa viumbe wake wenye akili ni wa kadiri tu. Ingawa Adamu aliumbwa akiwa mkamilifu, alipaswa kuheshimu mipaka aliyowekewa na Muumba wake. Kwa mfano, hangeweza kula udongo, changarawe, au mbao bila kupata matatizo. Ikiwa angepuuza sheria ya uvutano na kuruka kutoka mahali palipoinuka sana, angeweza kufa au kuumia vibaya.

      Vivyo hivyo, hakuna kiumbe mkamilifu—binadamu au malaika—anayeweza kupuuza kanuni ambazo zimewekwa na Mungu kuhusu mwenendo mzuri na asipatwe na matatizo. Hivyo, wakati kiumbe mwenye akili anapotumia vibaya uhuru wake wa kuamua, anaanguka kwa urahisi katika kosa na dhambi.—Mwanzo 1:29; Mathayo 4:4.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki