Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wachukiwa kwa Sababu ya Imani Yao
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Desemba 1
    • 22. (a) Ni kielelezo gani kionyeshacho kwamba Mashahidi wa Yehova hujitahidi sana ‘kufanya lililo jema kuelekea wote’? (Ona sanduku kwenye ukurasa wa 11.) (b) Ni nini kitakachozungumziwa katika makala inayofuata?

      22 Kama Wakristo wa mapema, Mashahidi wa Yehova wa nyakati za kisasa wamekuwa “vitu vya kuchukiwa” katika nchi mbalimbali. Hata hivyo, wao hawawachukii wasio Mashahidi; wala hawajapata kuanzisha maasi dhidi ya serikali. Kinyume cha hilo, wanajulikana ulimwenguni pote kwa kuonyesha upendo wa kweli ambao huvuka mipaka yote ya kijamii, kitaifa, na kikabila. Basi, ni kwa nini wamenyanyaswa? Nao huitikiaje upinzani? Maswali hayo yatazungumziwa katika makala inayofuata.

  • Kutetea Imani Yetu
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Desemba 1
    • Kutetea Imani Yetu

      “Mtakaseni Kristo kuwa Bwana katika mioyo yenu, sikuzote mkiwa tayari kujitetea mbele ya kila mtu ambaye hudai kwenu sababu ya tumaini lililo katika nyinyi.”—1 PETRO 3:15.

      1, 2. Kwa nini Mashahidi wa Yehova hawashangazwi na upinzani, lakini wao hutamani nini?

      KATIKA nchi zilizo nyingi, Mashahidi wa Yehova hujulikana na wengi kuwa watu wenye kufuata haki na walio safi kiadili. Wengi huwaona kuwa majirani wema wasiosababisha matatizo yoyote. Lakini, kinyume cha hilo, Wakristo hawa wapenda-amani wamenyanyaswa isivyo haki—nyakati za vita na za amani. Wao hawashangazwi na upinzani huo. Kwa kweli, wao huutarajia. Wanajua kwamba Wakristo waaminifu katika karne ya kwanza W.K. walikuwa “vitu vya kuchukiwa,” kwa hiyo, mbona wale wanaojitahidi kuwa wafuasi wa kweli wa Kristo leo watarajie kutendwa tofauti? (Mathayo 10:22) Isitoshe, Biblia husema: “Wote wale wanaotamani kuishi kwa ujitoaji-kimungu katika ushirika na Kristo Yesu watanyanyaswa pia.”—2 Timotheo 3:12.

      2 Mashahidi wa Yehova hawatafuti kunyanyaswa, wala hawafurahii shida—faini, vifungo, au kutendwa kikatili—ziwezazo kuletwa na mnyanyaso. Wao hutamani “kuishi maisha yaliyo shwari na matulivu” ili waweze kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu bila kizuizi. (1 Timotheo 2:1, 2) Wao huthamini uhuru wa kidini wa kuendelea na ibada yao walio nao katika nchi nyingi, nao hufanya kwa kudhamiria yale wawezayo “kufanya amani na watu wote,” kutia ndani watawala wa serikali za kibinadamu. (Waroma 12:18; 13:1-7) Kwa nini, basi, wao ni “vitu vya kuchukiwa”?

      3. Sababu moja inayofanya Mashahidi wa Yehova wachukiwe isivyo haki ni gani?

      3 Kusema kweli, Mashahidi wa Yehova wamechukiwa isivyo haki kwa sababu zilezile zilizofanya Wakristo wa mapema wanyanyaswe. Kwanza, Mashahidi wa Yehova hutenda kulingana na itikadi zao za kidini katika njia ambazo huwafanya wasipendwe na wengine. Kwa kielelezo, wao huhubiri kwa bidii habari njema ya Ufalme wa Mungu, lakini mara nyingi watu hukosa kuelewa bidii yao, wakiona kuhubiri kwao kuwa “kugeuza imani kwa jeuri.” (Linganisha Matendo 4:19, 20.) Wao pia hawajiingizi katika siasa na vita vya mataifa, na nyakati nyingine jambo hilo limechukuliwa kimakosa kumaanisha kwamba, Mashahidi si raia waaminifu-washikamanifu.—Mika 4:3, 4.

      4, 5. (a) Mashahidi wa Yehova wamekuwaje shabaha ya mashtaka yasiyo ya kweli? (b) Ni nani ambao mara nyingi wamekuwa wachochezi wakuu wa kunyanyaswa kwa watumishi wa Yehova?

      4 Pili, Mashahidi wa Yehova wamekuwa shabaha za mashtaka yasiyo ya kweli—uwongo ulio wazi na kuwasilishwa kulikopotoka kwa itikadi zao. Katika nchi fulani, hilo limefanya washambuliwe isivyo haki. Isitoshe, kwa sababu wao hutafuta matibabu yasiyohusisha damu ambayo hupatana na tamaa yao ya kutii amri ya Biblia ya ‘kujiepusha na damu,’ wameitwa isivyofaa “waua-watoto kimakusudi” na pia “madhehebu ya kujiua.” (Matendo 15:29) Lakini ukweli ni kwamba Mashahidi wa Yehova huthamini sana uhai, nao hutafuta kupata utunzaji wa kitiba bora zaidi ambao waweza kupatikana kwa ajili yao wenyewe na watoto wao. Shtaka la kwamba watoto wengi wa Mashahidi wa Yehova hufa kila mwaka kwa sababu ya kukataa kutiwa damu mishipani halina msingi wowote. Kwa kuongezea, kwa kuwa kweli ya Biblia haiwaathiri washiriki wa familia kwa kiwango kilekile, Mashahidi hulaumiwa pia kwa kuvunja familia. Hata hivyo, wale wanaowafahamu Mashahidi wa Yehova wanajua kwamba wao hustahi sana maisha ya familia na hujaribu kufuata amri za Biblia kwamba mume na mke wapendane na kustahiana na kwamba watoto wawatii wazazi wao, wawe waamini au la.—Waefeso 5:21–6:3.

      5 Katika visa vingi, wachochezi wakuu wa mnyanyaso wa watumishi wa Yehova wamethibitika kuwa wapinzani wa kidini ambao wametumia uwezo walio nao na wenye mamlaka na vyombo vya habari kujaribu kukandamiza utendaji wa Mashahidi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki