-
Walishinda Licha ya MatesoMnara wa Mlinzi—2003 | Machi 1
-
-
Frieda aliteswa kwa miaka 23 chini ya tawala mbili za kimabavu. “Wanazi walijaribu kuniangamiza; Wakomunisti nao wakajaribu kuniponda roho. Nilipataje nguvu ya kuvumilia? Nilijifunza Biblia kwa bidii nilipokuwa huru, nilisali nilipokuwa peke yangu, nilishirikiana na waamini wenzangu ilipowezekana, na niliongea na wengine kuhusu imani yangu nafasi ilipopatikana.”
-
-
Walishinda Licha ya MatesoMnara wa Mlinzi—2003 | Machi 1
-
-
Ádám alizidi kuonewa hadi katikati ya miaka ya 1970, hiyo ikiwa zaidi ya miaka 35 baada ya Wanafunzi wa Biblia kuwatembelea wazazi wake kwa mara ya kwanza. Katika kipindi hicho chote, mahakama sita zilimhukumu vifungo mbalimbali vya jumla ya miaka 23 katika angalau magereza na kambi kumi. Alivumilia mateso ambayo yaliendelezwa na tawala tatu, yaani, Wafashisti wa kabla ya vita ya pili ya ulimwengu nchini Hungaria, Wanazi nchini Serbia, na Wakomunisti wakati wa vita baridi nchini Hungaria.
Ádám angali anaishi mjini kwao, Paks, akimtumikia Mungu kwa uaminifu. Je, ana vipawa visivyo vya kawaida ambavyo vilimwezesha kuvumilia magumu kwa ushindi? La. Anaeleza:
“Funzo la Biblia, sala, na kushirikiana na waamini wenzangu, yalikuwa mambo muhimu. Lakini ningependa kukazia mambo mengine mawili. Kwanza, Yehova ndiye Chanzo cha nguvu. Uhusiano wa karibu naye ulikuwa msaada mkubwa kwangu. Na pili, nilikumbuka sura ya 12 ya Waroma, inayosema hivi: ‘Msijilipizie kisasi.’ Kwa hiyo, sikuweka kinyongo kamwe. Mara nyingi nilikuwa na nafasi ya kulipiza kisasi, lakini sikufanya hivyo kamwe. Hatupaswi kutumia nguvu ambayo Yehova anatupatia kulipa ovu kwa ovu.”
-