-
“Umati Mkubwa Ukamkaribia”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
13. Wazazi wanaweza kumwiga Yesu jinsi gani?
13 Haikuwa vigumu kwa watu kutambua kwamba Yesu anapendezwa nao binafsi. Hata alipokuwa chini ya hali ngumu hakuacha kupendezwa na watu. Kama tulivyoona, wazazi walipomletea watoto wao, Yesu alikubali wamkaribie hata alipokuwa na shughuli nyingi na madaraka mazito. Aliwawekea wazazi mfano mzuri kama nini! Si rahisi kulea watoto katika ulimwengu wa leo. Hata hivyo, watoto wanapaswa kujisikia huru wanapokuwa na wazazi wao. Ikiwa wewe ni mzazi, unajua kwamba kuna nyakati ambazo unaweza kuwa na shughuli nyingi usiweze kumpa mtoto wako uangalifu anaohitaji. Kwa nini usimwambie utatenga wakati haraka iwezekanavyo uwe pamoja naye? Ukitimiza ahadi yako, mtoto wako atajifunza faida ya kungoja. Pia, atajua kwamba wakati wowote anaweza kukueleza jambo lolote linalomhangaisha.
-
-
“Umati Mkubwa Ukamkaribia”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
Mwonyeshe mtoto wako kwamba anaweza kukukaribia na kwamba unamjali kikweli
16 Wazazi wanaweza kujifunza somo la maana katika kisa hicho pia. Namna gani mtoto wako akija kwako akiwa na tatizo fulani? Huenda ukaliona tatizo lake kuwa dogo. Labda hata unaweza kuliona kuwa jambo la kuchekesha. Kwa kulinganisha na matatizo yako, huenda kwa kweli tatizo la mtoto wako likaonekana kuwa dogo. Hata hivyo, kumbuka kwamba kwa mtoto wako si tatizo dogo! Ikiwa linamhangaisha mtu unayempenda sana, je, halipaswi kukuhangaisha pia? Kumwambia mtoto wako kwamba unajali mahangaiko yake kutafanya ajisikie huru kukukaribia.
-