-
Mafundisho ya Kimungu Huwa na Matokeo MazuriAmkeni!—2007 | Agosti
-
-
Dorian, kijana kutoka Peru, Amerika Kusini, alitoa hotuba yake ya kwanza katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova alipokuwa na umri wa miaka minne. Alipoanza kwenda shule, angeweza kutumia Biblia kumweleza mwalimu na wanafunzi wenzake kwa nini yeye hasherehekei Krismasi.
Hivi karibuni, alipokuwa na umri wa miaka mitano, Dorian aliombwa atoe hotuba mbele ya shule nzima, yaani, mbele ya wanafunzi 500 hivi na kueleza maoni yake kuhusu Sikukuu ya Akina Baba. Alitayarisha hotuba ya dakika kumi yenye kichwa “Madaraka ya Baba,” ikitegemea Waefeso 6:4. Mwisho wa hotuba yake alisema, “Badala ya kusherehekea Sikukuu ya Akina Baba siku moja kwa mwaka, watoto wanapaswa kuwaheshimu na kuwatii wazazi wao kila siku.”
-
-
Mafundisho ya Kimungu Huwa na Matokeo MazuriAmkeni!—2007 | Agosti
-
-
[Picha katika ukurasa wa 28]
Dorian akiwa shuleni
-