Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Barua ya Yakobo na ya Petro
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
    • Kabla tu ya kampeni ya kuwatesa Wakristo ya Maliki Mroma Nero mwaka wa 64 W.K., mtume Petro anawaandikia Wakristo barua yake ya kwanza ili kuwatia moyo wasimame imara katika imani.

  • Mambo Makuu Katika Barua ya Yakobo na ya Petro
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
    • ‘SIMAMA IMARA KATIKA IMANI’

      (1 Pet. 1:1–5:14)

      Petro anawakumbusha waamini wenzake kuhusu “tumaini lililo hai” la urithi mbinguni. Petro anawaambia hivi: “Ninyi ni ‘jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu.’” Baada ya kutoa mashauri hususa kuhusu kujitiisha, anawahimiza wote kuwa na ‘akili zinazopatana, wakionyesha hisia-mwenzi, wakiwa na upendo wa kindugu, wenye huruma nyororo, wanyenyekevu katika akili.’—1 Pet. 1:3, 4; 2:9; 3:8.

      Kwa kuwa “mwisho wa [mfumo wa Kiyahudi wa] mambo umekaribia,” Petro anawashauri ndugu ‘wawe na utimamu wa akili, na kukesha kuhusiana na sala.’ Anawaambia hivi: “Tunzeni akili zenu, iweni wenye kulinda. . . . Chukueni msimamo mkampinge [Shetani], mkiwa imara katika imani.”—1 Pet. 4:7; 5:8, 9.

      Maswali ya Kimaandiko Yajibiwa:

      3:20-22—Ubatizo unatuokoa jinsi gani? Ubatizo ni takwa kwa wale wanaotafuta wokovu. Hata hivyo, ubatizo peke yake hautuokoi. Wokovu ni “kupitia ufufuo wa Yesu Kristo.” Mtu anayebatizwa anapaswa kuamini kwamba wokovu unawezekana tu kwa sababu Yesu alikufa kifo cha kidhabihu, akafufuliwa, na ‘yuko kwenye mkono wa kuume wa Mungu,’ akiwa na mamlaka juu ya watu walio hai na wafu. Ubatizo unaotegemea imani kama hiyo ndio ambao unalingana na ‘nafsi nane, waliochukuliwa salama kupitia maji.’

      4:6—Ni nani “wafu” ambao ‘walitangaziwa habari njema’? Hao ni wale ambao walikuwa ‘wafu katika makosa yao na dhambi zao,’ au wale ambao walikuwa wafu kiroho, kabla ya kusikia habari njema. (Efe. 2:1) Hata hivyo, baada ya kuamini habari njema, walianza kuwa “hai” kiroho.

      Mambo Tunayojifunza:

      1:7. Ili imani yetu iwe na thamani kubwa, ubora wake unapaswa kujaribiwa. Imani kama hiyo yenye nguvu ndiyo kwa kweli ‘inayohifadhi hai nafsi.’ (Ebr. 10:39) Hatupaswi kurudi nyuma imani yetu inapojaribiwa kwa njia mbalimbali.

      1:10-12. Malaika walitamani sana kuchunguza na kuelewa kweli nzito za kiroho ambazo manabii wa Mungu wa zamani waliandika kuhusu kutaniko la Kikristo la watiwa-mafuta. Hata hivyo, mambo hayo yalieleweka waziwazi Yehova alipoanza kushughulika na kutaniko. (Efe. 3:10) Je, hatupaswi kufuata mfano wa malaika na kujitahidi kuchunguza ndani ya “mambo mazito ya Mungu”?—1 Kor. 2:10.

      2:21. Kwa kumwiga Yesu Kristo, ambaye ndiye Kielelezo chetu, tunapaswa kuwa tayari kuteseka hata kufikia kifo ili kuunga mkono enzi kuu ya Yehova.

      5:6, 7. Tunapomtupia Yehova mahangaiko yetu, anatusaidia tuendelee kutanguliza ibada ya kweli katika maisha yetu badala ya kuhangaikia sana mambo ya kesho.—Mt. 6:33, 34.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki