-
Shauri la Yehova Dhidi ya MataifaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
“Joka la Moto Arukaye” Dhidi ya Ufilisti
4. Ni yapi baadhi ya mambo makuu ya tangazo la Yehova dhidi ya Ufilisti?
4 Wafilisti wazingatiwa kwanza. “Ufunuo huu ulikuja mwaka ule alipokufa mfalme Ahazi. Usifurahi, Ee Ufilisti, pia wote, kwa sababu fimbo ile iliyokupiga imevunjika; maana katika shina la nyoka atatoka fira, na uzao wake ni joka la moto arukaye.”—Isaya 14:28, 29.
5, 6. (a) Uzia alikuwaje kama nyoka kwa Wafilisti? (b) Hezekia athibitika kuwa nini dhidi ya Ufilisti?
5 Mfalme Uzia alikuwa na nguvu za kutosha kuzuia tisho la Ufilisti. (2 Mambo ya Nyakati 26:6-8) Machoni pao, Uzia alikuwa kama nyoka, na fimbo yake ilimpiga-piga jirani huyo mwenye uadui. Baada ya kifo cha Uzia—‘fimbo yake ilivunjika’—Yothamu mwaminifu akatawala, ingawa “watu waliendelea kufanya maovu.” Kisha Ahazi akawa mfalme. Hali ikabadilika, na Wafilisti wakafanya mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Yuda kwa mafanikio. (2 Mambo ya Nyakati 27:2, BHN; 28:17, 18) Hata hivyo, sasa hali yabadilika tena. Mfalme Ahazi afa mwaka wa 746 K.W.K., na Hezekia mchanga achukua kiti cha ufalme. Iwapo Wafilisti wafikiri kuwa hali yao itaendelea kuwa shwari, basi wamekosea kabisa. Hezekia athibitika kuwa adui motomoto. Hezekia, aliye mzao wa Uzia (“uzao” kutoka katika “shina” lake), ni kama “joka la moto arukaye”—huku akipiga mbio kwenda kushambulia kwa haraka, na kutokeza madhara makali, kana kwamba anawadunga majeruhi wake sindano ya sumu.
6 Huo ni ufafanuzi ufaao kuhusu mfalme huyo mpya. Hezekia ndiye ‘aliyewapiga Wafilisti mpaka Gaza na mipaka yake.’ (2 Wafalme 18:8) Kwa mujibu wa kumbukumbu za kihistoria za Mfalme Senakeribu wa Ashuru, Wafilisti waja kutiishwa chini ya Hezekia. “Walio maskini”—ufalme wa Yuda uliofifia—wapata kufurahia usalama na wingi wa mali, huku Ufilisti ikidhikika kwa njaa.—Soma Isaya 14:30, 31.
-
-
Shauri la Yehova Dhidi ya MataifaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
8. (a) Mataifa fulani leo yamekuwaje kama Ufilisti? (b) Yehova amefanya nini ili kuwasaidia watu wake leo, kama alivyofanya nyakati za kale?
8 Sawa na Ufilisti, mataifa fulani leo huwapinga vikali waabudu wa Mungu. Mashahidi Wakristo wa Yehova wametupwa magerezani na katika kambi za mateso. Wamepigwa marufuku. Baadhi yao wameuawa. Wapinzani wazidi ‘kuishambulia nafsi yake mwenye haki.’ (Zaburi 94:21) Machoni pa adui zao, kikundi hicho cha Wakristo huenda kikaonekana kuwa “maskini” na “wahitaji.” Hata hivyo, kwa msaada wa Yehova, wao hufurahia chakula kingi cha kiroho, huku adui zao wakidhikika kwa njaa. (Isaya 65:13, 14; Amosi 8:11) Yehova atakaponyosha mkono wake dhidi ya Wafilisti wa siku za kisasa, “maskini” hao watakuwa salama. Wapi? Kwa kushirikiana na ‘nyumba ya Mungu,’ ambamo Yesu ndiye jiwe la pembeni la msingi lililo thabiti. (Waefeso 2:19, 20) Nao watakuwa chini ya ulinzi wa “Yerusalemu la kimbingu,” Ufalme wa Yehova wa mbinguni, ambapo Yesu Kristo ndiye Mfalme wake.—Waebrania 12:22; Ufunuo 14:1.
-