Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Origen—Mafundisho Yake Yaliathirije Kanisa?
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Julai 15
    • Wengi wa wanafunzi wake walikuwa wakipambana na masuala ya kifalsafa ya wakati wao. Katika jitihada ya kuwasaidia, Origen alichunguza kwa uangalifu wafuasi mbalimbali wa falsafa waliokuwa wakielekeza akili za wanafunzi wake wachanga. Alikusudia kujibu maswali ya kifalsafa ya wanafunzi wake kwa njia yenye kuridhisha.

      Katika jitihada ya kupatanisha Biblia na falsafa, Origen alitumia sana njia ya kufasiri Maandiko kwa kuzingatia maana iliyositiriwa ya kiroho. Alikata kauli kwamba sikuzote Maandiko yana maana iliyositiriwa ya kiroho na si lazima yawe na maana halisi. Kama alivyosema msomi mmoja, jambo hilo lilimpa Origen “uwezo wa kuyapa maana ya Biblia mawazo yoyote yasiyo ya Biblia yaliyokubaliana na mfumo wake wa kitheolojia, huku akidai (na bila shaka akijiona mwenyewe kwa unyofu) kuwa mfasiri mwenye bidii na mwaminifu wa mawazo ya Biblia.”

      Barua moja ambayo Origen alimwandikia mmoja wa wanafunzi wake yaeleza kwa kina kufikiri kwake. Origen alisema kwamba Waisraeli walitengeneza vyombo vya hekalu la Yehova kwa kutumia dhahabu ya Misri. Kwa kutumia mfano huo, yeye pia angeweza kutumia falsafa ya Kigiriki kufundisha Ukristo. Aliandika hivi: “Jinsi wana wa Israeli walivyofaidika kwa vitu walivyotoa Misri, ambavyo Wamisri hawakuvitumia ifaavyo, lakini Waebrania wakiongozwa na hekima ya Mungu, wakavitumia katika utumishi wa Mungu.” Kwa hiyo Origen aliwatia moyo wanafunzi wake ‘watwae habari zozote kutoka katika falsafa ya Kigiriki na kuzitumia kujitayarishia Ukristo.’

      Njia hii isiyo na mipaka ya kufasiri Biblia, ilifanya iwe vigumu sana kutofautisha mafundisho ya Kikristo na falsafa ya Kigiriki. Kwa mfano, katika kitabu chake chenye kichwa On First Principles, Origen alimfafanua Yesu kuwa ‘Mwana mzaliwa-pekee, aliyezaliwa, lakini asiye na mwanzo.’ Aliongezea hivi: ‘Uzaliwa wake ni wa umilele. Hakuwa Mwana kwa sababu ya kupokea pumzi ya uhai, wala si kupitia tendo jinginelo, bali kwa asili ya Mungu mwenyewe.’

      Origen hakupata wazo hilo katika Biblia, kwa kuwa Maandiko hufundisha kwamba Mwana pekee wa Yehova ni “mzaliwa wa kwanza wa uumbaji wote” na “mwanzo wa uumbaji wa Mungu.” (Wakolosai 1:15; Ufunuo 3:14) Kulingana na mwanahistoria wa dini Augustus Neander, Origen alifikia uamuzi wa dhana ya “uzaliwa wa umilele” kupitia “elimu yake ya kifalsafa katika shule ya Plato.” Kwa hiyo, Origen alikiuka kanuni hii ya Kimaandiko iliyo ya msingi: “Msiyapite mambo ambayo yameandikwa.”—1 Wakorintho 4:6.

  • Origen—Mafundisho Yake Yaliathirije Kanisa?
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Julai 15
    • Kwa kuchanganya mafundisho ya Biblia na falsafa ya Kigiriki, theolojia ya Origen ilijaa makosa, na matokeo yakawa mabaya sana kwa Jumuiya ya Wakristo. Kwa mfano, ijapokuwa makisio mengi ya ajabu-ajabu ya Origen yalikataliwa baadaye, maoni ya Origen juu ya “uzaliwa wa umilele” wa Kristo yalisaidia kuweka msingi wa fundisho lisilo la Biblia la Utatu. Kitabu The Church of the First Three Centuries chasema hivi: “Watu wangezidi kupendelea falsafa [iliyoanzishwa na Origen] kwa muda mrefu.” Kukiwa na matokeo gani? “Ule usahili wa imani ya Kikristo ulichafuliwa, na makosa mengi sana yakaingia katika Kanisa.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki