-
Baraka za Huduma ya PainiaMnara wa Mlinzi—1997 | Oktoba 15
-
-
5 Haishangazi kwamba, wale wanaoshiriki katika huduma ya wakati wote mara nyingi huelezea shangwe na hisi yenye kina ya utimizo wanayopata kutokana na huduma yao. “Najua kwamba hakuna kazi nyingine ambayo ingeweza kuniletea utoshelezo unaotokana na kushiriki kweli na wengine,” asema painia mwenye umri wa miaka 64 kutoka Uingereza. Mjane kutoka Zaire alieleza kile ambacho kupainia kumemaanisha kwake: “Utumishi wa painia ulikuwa faraja kwangu baada ya kumpoteza mume wangu mpendwa. Kadiri ninapoenda katika utumishi kusaidia wengine, ndivyo huzuni yangu inapopungua. Naweka imani yangu katika ahadi za Yehova na kufikiri zaidi jinsi ninavyoweza kusaidia wale ninaojifunza nao wafanye mabadiliko katika maisha zao. Mwishoni mwa kila siku, usingizi wangu ni mtamu na moyo wangu umejawa shangwe.”
6. Ni shangwe gani za pekee ambazo baadhi ya mapainia wameziona?
6 Baadhi ya watu ambao wamekuwa wakipainia kwa miongo mingi wamekuwa na shangwe ya pekee ya kutumikia maeneo ya mbali sana, wakianzisha makutaniko, ambayo hatimaye yalikua hadi kufikia kuwa mizunguko. Kwa mfano, katika Abashiri, Hokkaido (kisiwa cha kusini sana mwa Japani), kuna dada ambaye amekuwa akipainia kwa miaka 33. Anakumbuka kwamba kwenye kusanyiko lake la kwanza la mzunguko—Hokkaido yote—kulikuwa na hudhurio la watu 70 tu. Na sasa? Kuna mizunguko 12 kwenye kisiwa hicho, kukiwa na jumla ya wahubiri 12,000. Wazia jinsi ambavyo moyo wake hufurika kwa shangwe anapohudhuria makusanyiko na mikusanyiko pamoja na songamano la wapiga-mbiu wa Ufalme wenzake kwenye kisiwa hicho!
7, 8. Ni shangwe gani ambayo mapainia walio wengi wa muda mrefu wameona?
7 Mapainia wengine wa muda mrefu wamekuwa na shangwe ya kuona wanafunzi wa Biblia wakibatizwa kisha wakifikia mapendeleo makubwa zaidi ya utumishi. Katika Japani dada ambaye ametumikia kwa migawo tisa tofauti ya painia tangu 1957 akumbuka akimwangushia mwanamke mmoja mchanga gazeti la Amkeni! aliyekuwa akifanya kazi benki. Mwanamke huyo alibatizwa kati ya muda wa miezi tisa. Baadaye aliolewa, na yeye na mume wake wakawa mapainia wa pekee. Ilikuwa shangwe kama nini kwa dada huyo painia, wakati, akiwa katika mgawo wake wa tatu, kutaniko lake lilipotembelewa na mwangalizi wake mpya wa mzunguko pamoja na mke wake—mwanafunzi wake wa zamani wa Biblia!
8 Si ajabu kwamba wale ambao wamefanya huduma ya painia kuwa kazi-maisha yao wanaoiona kuwa “pendeleo lenye thamani sana la kuthaminiwa,” kama alivyoeleza painia mmoja wa muda wa miaka 22!
-
-
Baraka za Huduma ya PainiaMnara wa Mlinzi—1997 | Oktoba 15
-
-
10, 11. Kutokana na mambo yaliyoonwa, mapainia wengi wanajua jambo gani kuhusu uwezo wa Yehova wa kuandaa?
10 Mapainia ulimwenguni pote wanajua kutokana na mambo waliyojionea kwamba Yehova huandalia wale wanaojiweka katika mikono yake ya utunzaji. Fikiria kisa cha wenzi wa ndoa mapainia ambao walihamia mji mdogo ambapo kulikuwa na uhitaji wa wahubiri wa Ufalme. Baada ya miezi michache, kazi ya kimwili ikawa haipatikani, na fedha zao walizokuwa wameweka zilimalizika kabisa. Kisha walipokea hati ya malipo ya bima ya gari ya dola 81. “Hatukuwa na njia ya kuilipia,” aeleza ndugu huyo. “Tulisali sana usiku huo.” Siku iliyofuata, walipokea kadi kutoka kwa familia ambayo wao wenyewe walikuwa wanapambana kifedha. Familia hiyo ilikuwa imepokea fedha za kodi zinazorudishwa, kadi hiyo ilieleza, na kwa kuwa zilikuwa nyingi kuliko walivyotazamia, walitaka kushiriki baadhi yake na wenzi wa ndoa mapainia. Pamoja nayo, iliandamanishwa hundi ya dola 81! “Sitasahau kamwe siku hiyo—nywele katika shingo langu zilisimama wima!” asema ndugu painia. “Tulithamini sana ukarimu wa familia hii.” Pia Yehova huthamini fadhili ya aina hiyo, ambayo yafanana na roho ya ukarimu anayotia moyo watumishi wake kuwa nayo.—Mithali 19:17; Waebrania 13:16.
11 Mapainia wengi wanaweza kusimulia mambo yaliyoonwa yaliyo sawa na hayo. Waulize, nao watakuambia kwamba “hawakuachwa kabisa.” Akitazama nyuma baada ya miaka 55 ya huduma ya wakati wote, painia mwenye umri wa miaka 72 asema, “Yehova hakunisikitisha kamwe.”—Waebrania 13:5, 6.
-
-
Baraka za Huduma ya PainiaMnara wa Mlinzi—1997 | Oktoba 15
-
-
13. Wengine wanasema nini kuhusu tokeo la huduma yao ya painia na uhusiano wao na Yehova?
13 Mapainia wanaweza kutumia wakati mwingi kila mwezi katika kujifunza kuhusu Yehova na kufundisha kumhusu. Wanahisi kwamba hilo huathirije uhusiano wao na Mungu? “Kupainia ni njia bora kabisa ya kumkaribia Yehova,” ajibu mzee katika Ufaransa ambaye amekuwa akipainia kwa miaka zaidi ya kumi. Painia mwingine katika nchi hiyo, ambaye ametumia miaka 18 katika huduma ya wakati wote, asema: “Utumishi wa painia huturuhusu ‘kuonja tuone ya kwamba Yehova ni mwema,’ siku baada ya siku tukijenga uhusiano wenye nguvu hata zaidi pamoja na Muumba wetu.” (Zaburi 34:8) Dada mmoja Uingereza ambaye amekuwa akipainia kwa miaka 30 anahisi vivyo hivyo. “Kupata mwongozo wa roho ya Yehova katika huduma hunileta karibu naye,” yeye asema. “Kwa kweli nimehisi kwamba roho ya Yehova katika pindi nyingi imeniongoza kwenye nyumba mahususi kwa wakati ufaao.”—Linganisha Matendo 16:6-10.
14. Mapainia wananufaikaje kwa kutumia Biblia na vichapo vya Biblia siku baada ya siku kufundisha wengine?
14 Mapainia wengi huona kwamba kutumia Biblia na vichapo vya Biblia siku baada ya siku ili kueleza na kufundisha kweli za Maandiko huwasaidia wakue katika ujuzi wa Neno la Mungu. Ndugu mwenye umri wa miaka 85 katika Hispania ambaye amepainia kwa miaka 31 aeleza: “Kupainia kumenisaidia kujipatia ujuzi wa Biblia wenye kina, ujuzi ambao lazima nitumie ili kusaidia watu wapate kumjua Yehova na makusudi yake.” Dada kutoka Uingereza ambaye amekuwa akipainia kwa miaka 23 asema: “Huduma ya wakati wote imenisaidia kusitawisha hamu ya moyoni ya chakula cha kiroho.” Kuelezea wengine “sababu ya tumaini lililo katika [wewe]” kwaweza kuimarisha usadikisho wako mwenyewe kuhusu itikadi unazozipenda sana. (1 Petro 3:15) Painia kutoka Australia asema hivi: “Kupainia huboresha imani yangu ninapojieleza kwa wengine.”
-