-
Je, Wewe ni Painia Mwenye Usawaziko?Mnara wa Mlinzi—1996 | Mei 15
-
-
Kumiko amekuwa painia kwa miongo miwili. Ingawa ana watoto watatu na mume asiyeamini, amegundua kutokana na mambo aliyojionea kuwa wakati umfaao kuisoma Biblia ni kabla tu ya kwenda kitandani. Ajifunzapo, yeye hasa huandika hoja awezazo kutumia katika huduma ya shambani ili aweze kufanya huduma yake ya kila siku iwe mpya na ya kupendeza. Mapainia wengine wenye mafanikio huamka kabla ya wengine katika familia kuamka ili kujilisha kiroho wakati wa zile saa za asubuhi zenye utulivu. Huenda ukawa na nyakati nyingine zifaazo zilizowekwa kando kwa ajili ya kutayarisha mikutano na kusoma vichapo vya karibuni zaidi vya Kikristo. Ukitamani kudumisha shangwe ya huduma, funzo la kibinafsi si jambo liwezalo kufanywa haraka-haraka au kupuuzwa.
-
-
Je, Wewe ni Painia Mwenye Usawaziko?Mnara wa Mlinzi—1996 | Mei 15
-
-
Mapainia wengi hujitahidi kuhubiri sana wakati washiriki wa familia hawako nyumbani. Kumiko, aliyetajwa mapema, huwa na familia yake wakila kiamsha kinywa, huaga mume na watoto wake asubuhi waondokapo naye hurudi nyumbani kabla hawajarejea. Yeye hutumia siku za Jumatatu ili kupika vyakula mbalimbali mapema ili aweze kupumzika na kula milo pamoja na familia yake badala ya kujishughulisha mno jikoni. Kufanya zaidi ya kazi moja kwa wakati mmoja, kama vile kazi nyingine za nyumbani huku akitayarisha milo, pia husaidia. Kwa njia hiyo Kumiko hata hupata nafasi ya kukaribisha marafiki wa watoto wake nyumbani na kuwaandalia vitu vya kuwafurahisha.
Watoto wakuapo na kuingia katika miaka yao ya utineja, mara nyingi wao huhitaji uangalifu mwingi kutoka kwa wazazi katika kukabiliana na mambo mapya yawakumbayo kama hisia, tamaa, shaka, na woga. Hili hutaka mzazi aliye painia awe chonjo na kubadili ratiba. Mfikirie Hisako, painia aliye mama ya watoto watatu. Yeye alifanya nini wakati binti yake mkubwa zaidi alipoanza kukosa shangwe na uchangamfu kwa ajili ya mikutano ya Kikristo na huduma ya shambani kwa sababu ya uvutano wa marafiki walimwengu shuleni? Uhitaji halisi ulikuwa binti yake kuufanya ukweli kuwa wake mwenyewe na kuwa na hakika kabisa kuwa kujitenga na ulimwengu ndiyo njia bora zaidi.—Yakobo 4:4.
Hisako asema: “Niliamua kujifunza tena naye mafundisho ya msingi katika kitabu Kuishi Milele kila siku. Mwanzoni tuliweza kujifunza kwa dakika chache tu, mara nyingi binti yangu akilalamika kuwa na maumivu makali ya tumbo na kichwa wakati wa funzo ulipofika. Lakini niliongoza hilo funzo kwa ukawaida. Baada ya miezi michache, mwelekeo wake ulibadilika sana, ukielekeza kwenye kujiweka kwake wakfu na kubatizwa baada ya muda mfupi.” Sasa Hisako anafurahia huduma ya wakati wote pamoja na binti yake.
-