-
Samoa2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
KUSHINDA MATATIZO YA AFYA ILI KUMTUMIKIA YEHOVA
Mmoja wao ni Metusela Neru. Alipokuwa na umri wa miaka 12, alianguka alipokuwa akiendesha farasi na kuvunjika mgongo. “Baada ya kuanguka,” akumbuka mmishonari mmoja, “alitembea kana kwamba ana kibiongo, naye alikuwa na maumivu daima.” Metusela alipoanza kujifunza Biblia akiwa na umri wa miaka 19, aliamua kabisa kuvumilia upinzani wa familia yake. Kwa sababu ya ulemavu wake, safari ya kwenda kwenye mikutano ambayo kwa kawaida ingechukua dakika tano, ilimchukua dakika 45, tena kwa shida. Hata hivyo, Metusela alifanya maendeleo, akabatizwa mwaka wa 1990. Baadaye akawa painia wa kawaida na kustahili kuwa mzee kutanikoni. Tangu wakati huo, watu zaidi ya 30 kutoka katika familia yao wamehudhuria mikutano huko faga, na baadhi yao wamebatizwa. Leo, licha ya matatizo yake ya afya, Metusela anajulikana kuwa mtu mwenye tabasamu na furaha sikuzote.
-
-
Samoa2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 115]
Metusela Neru
-