-
Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Msumbiji
Mnamo Agosti 2008, koti lilianguka kutoka kwenye gari lililokuwa likipita karibu na nyumba ya dada mmoja mjane na maskini. Dada huyo alipoliokota, alipata katika mifuko ya koti hilo karatasi fulani, vifuko vitatu vidogo vyenye vito vya bei ghali, na dola zipatazo 1,000. Alitafuta mtu ambaye angeweza kupiga nambari za simu zilizokuwa katika karatasi hizo ili kumwarifu aliyelipoteza koti hilo. Jioni hiyo, gari lenye wanaume wanne lilifika katika kijiji hicho. Mbele ya wenye mamlaka kijijini, dada yetu alimkabidhi mwenye koti, koti lake likiwa na kila kitu. Mwenye koti alianza kutokwa na machozi na kusema ikiwa lingeokotwa na mtu mwingine yeyote ambaye si Shahidi wa Yehova, hangepata chochote. Dada yetu mwaminifu, alitoa ushahidi katika kijiji hicho, ushahidi ambao ulimletea sifa nyingi Mungu wake, Yehova.
-
-
Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 46]
Uaminifu wake ulikuwa ushahidi
-