-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Tatu na cha Nne cha ZaburiMnara wa Mlinzi—2006 | Julai 15
-
-
“MTOLEENI SHUKRANI, LIBARIKINI JINA LAKE”
Fikiria sababu mbalimbali za kumtukuza Yehova zinazotajwa katika mkusanyo wa nne wa zaburi. Katika Zaburi ya 90, Musa analinganisha kuwapo kwa “Mfalme wa umilele” na maisha mafupi ya mwanadamu. (1 Timotheo 1:17) Kulingana na Zaburi 91:2, Musa anamwita Yehova ‘kimbilio na ngome yake,’ yaani, Chanzo cha usalama wake. Zaburi chache zinazofuata zinazungumzia sifa nzuri za Mungu, fikira zake zilizotukuka, na kazi zake za ajabu. Nyimbo tatu zinaanza kwa maneno haya, ‘Yehova mwenyewe amekuwa mfalme.’ (Zaburi 93:1; 97:1; 99:1) Kwa kusema kwamba Yehova ni Mtengenezaji wetu, mtunga-zaburi anatualika ‘tumtolee shukrani na kulibariki jina lake.’—Zaburi 100:4.
Mtawala anayemwogopa Yehova anapaswa kusimamiaje mambo? Zaburi ya 101 iliyoandikwa na Mfalme Daudi inajibu. Zaburi inayofuata inasema kwamba Yehova “hakika ataielekea sala ya wale waliovuliwa kila kitu, naye hataidharau sala yao.” (Zaburi 102:17) Zaburi ya 103 huonyesha fadhili zenye upendo na rehema za Yehova. Akirejelea vitu vingi vya Mungu hapa duniani, mtunga-zaburi anasema hivi kwa mshangao: “Jinsi kazi zako zilivyo nyingi, Ee Yehova! Zote umezifanya kwa hekima.” (Zaburi 104:24) Nyimbo mbili za mwisho za Kitabu cha Nne zinamtukuza Yehova kwa kazi zake za ajabu.—Zaburi 105:2, 5; 106:7, 22.
-
-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Tatu na cha Nne cha ZaburiMnara wa Mlinzi—2006 | Julai 15
-
-
“Msifuni Yah!”
Nyimbo tatu za mwisho katika Kitabu cha Nne cha Zaburi zinamalizia kwa kusihi hivi: “Msifuni Yah!” Zaburi ya mwisho pia inaanza kwa maneno hayo. (Zaburi 104:35; 105:45; 106:1, 48) Maneno “Msifuni Yah!” yanapatikana mara nyingi katika Kitabu cha Nne cha Zaburi.
Bila shaka, tuna sababu za kumsifu Yehova. Zaburi ya 73 hadi ya 106 zimetupa mambo mengi ya kutafakari na kujaza mioyo yetu shukrani kwa Baba yetu wa mbinguni. Tunapofikiria yale ambayo ametufanyia na atakayotufanyia wakati ujao, je, hatuchochewi ‘kumsifu Yah’ kwa nguvu zetu zote?
-