-
Jinsi ya Kumkaribia “Msikiaji wa Sala”Mnara wa Mlinzi—2006 | Septemba 1
-
-
17. Yehova hukubali sala za nani?
17 Mungu hakubali sala zote. Basi, tunawezaje kusali tukiwa na uhakika kwamba sala zetu zitakubaliwa? Watu waaminifu ambao Mungu aliwasikiliza zamani walimkaribia kwa unyoofu na kwa nia nzuri. Walionyesha kwamba wana imani kwa kutenda mema. Tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atawasikiliza wale wanaomkaribia kwa njia hiyohiyo leo.
18. Wakristo wanapaswa kutimiza takwa gani ili sala zao zisikiwe?
18 Kuna takwa lingine. Mtume Paulo alieleza takwa hilo, aliposema: “Kupitia yeye, sisi, . . . tunaweza kumkaribia Baba kwa roho moja.” Paulo alikuwa akizungumza juu ya nani alipoandika maneno haya, “kupitia yeye”? Alimaanisha Yesu Kristo. (Waefeso 2:13, 18) Naam, tunaweza kumkaribia Baba kwa uhuru kupitia Yesu tu.—Yohana 14:6; 15:16; 16:23, 24.
-
-
“Maombi Yenu na Yajulishwe Mungu”Mnara wa Mlinzi—2006 | Septemba 1
-
-
2. Ni jambo gani linalohitajiwa ili Mungu akubali sala?
2 Hata hivyo, huenda mtu akauliza, ‘Mungu hukubali sala za aina gani?’ Biblia inaeleza jambo moja ambalo linahitajiwa ili sala zikubaliwe: “Bila imani haiwezekani kamwe kumpendeza vema, kwa maana yule anayemkaribia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko na kwamba yeye huwa mthawabishaji wa wale wanaomtafuta kwa bidii.” (Waebrania 11:6) Naam, kama ilivyoelezwa katika makala iliyotangulia, imani ni takwa muhimu la kumkaribia Mungu. Mungu yuko tayari kukubali sala za wale wanaomkaribia, lakini ni lazima wawe na imani wanapofanya hivyo, watende mema, wawe wanyoofu, na wawe na nia nzuri.
-