-
Aokolewa Asiliwe na Simba!Sikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
NJAMA YA UUAJI YAANZA KUTEKELEZWA
7. Mawaziri na maliwali walimpendekezea mfalme nini, nao walifanyaje hivyo?
7 Dario alifikiwa na msafara wa mawaziri na maliwali ‘waliokusanyika pamoja mbele ya mfalme.’ Usemi wa Kiaramu unaotumiwa hapa una wazo la rabsharabsha zenye kelele. Yaonekana kwamba watu hao walifanya ionekane kana kwamba walikuwa na jambo la dharura la kumwambia Dario. Huenda walifikiri kwamba hangezusha maswali juu ya pendekezo lao ikiwa wangemwambia kwa usadikisho na kana kwamba ni jambo lililohitaji kuchukuliwa hatua mara moja. Kwa hiyo, wakataja jambo hilo moja kwa moja, wakisema: “Mawaziri wote wa ufalme, na manaibu, na maamiri, na madiwani, na maliwali wamefanya shauri pamoja ili kuweka amri ya kifalme; na kupiga marufuku, ya kwamba mtu ye yote atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme atatupwa katika tundu la simba.”a—Danieli 6:6, 7.
8. (a) Kwa nini Dario angeona sheria iliyopendekezwa kuwa yenye kupendeza? (b) Mawaziri na maliwali walikusudia nini hasa?
8 Rekodi za kihistoria zathibitisha kwamba lilikuwa jambo la kawaida kwa wafalme wa Mesopotamia kuonwa na kuabudiwa kama miungu. Kwa hiyo, bila shaka Dario alipendezwa na pendekezo hilo. Pia huenda jambo hilo lilionekana kuwa lenye faida. Kumbuka kwamba Dario alikuwa mgeni kwa watu waliokuwa wakiishi Babiloni. Sheria hiyo mpya ingemwimarisha akiwa mfalme, nayo ingechochea halaiki za watu waliokuwa wakiishi Babiloni wawe waaminifu na kuunga mkono serikali hiyo mpya. Ingawa hivyo, mawaziri na maliwali hawakupendezwa na hali nzuri ya mfalme walipokuwa wakipendekeza amri hiyo. Kusudi lao la kweli lilikuwa kumnasa Danieli, kwa kuwa walijua kwamba ilikuwa desturi yake kusali kwa Mungu mara tatu kwa siku kwenye madirisha yaliyo wazi katika chumba chake cha paa.
9. Kwa nini sheria hiyo mpya haingewatatiza watu wengi wasio Wayahudi?
9 Je, kizuizi hicho cha sala kingetatiza jumuiya zote za kidini za Babiloni? Sivyo, hasa kwa kuwa katazo hilo lingedumu mwezi mmoja tu. Isitoshe, ni watu wachache sana wasio Wayahudi ambao wangeona kuabudu mwanadamu kwa muda kuwa kuridhiana. Msomi mmoja wa Biblia ataarifu hivi: “Kumwabudu mfalme kulikuwa kawaida kwa mataifa hayo yenye kuabudu sanamu sana; na kwa hiyo Wababiloni walipoagizwa wamwabudu mshindi—Dario Mmedi—kama mungu, walikubali mara moja kufanya hivyo. Wayahudi peke yao ndio walioudhika na dai hilo.”
10. Wamedi na Waajemi waliionaje sheria iliyotungwa na mfalme wao?
10 Vyovyote vile, wageni wa Dario walimhimiza ‘apige marufuku, akatie sahihi maandiko hayo, yasibadilike, kama ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi, isiyoweza kubadilika.’ (Danieli 6:8) Katika Mashariki ya kale, mapenzi ya mfalme yalionwa kuwa sheria kamili. Hilo lilitokeza dhana ya kwamba hangeweza kukosea. Hata sheria ambayo ingesababisha vifo vya watu wasio na hatia ilipaswa kuendelea kutumika!
11. Danieli angeathiriwaje na amri iliyotolewa na Dario?
11 Bila kumfikiria Danieli, Dario akatia sahihi amri hiyo. (Danieli 6:9) Kwa kufanya hivyo, alitia sahihi hati ya kuidhinisha kifo cha waziri wake aliyemthamini zaidi. Ndiyo, bila shaka Danieli angeathiriwa na amri hiyo.
DARIO ALAZIMIKA KUTOA HUKUMU KALI
12. (a) Danieli alifanya nini mara tu alipopata kujua juu ya sheria hiyo mpya? (b) Ni nani waliokuwa wakimtazama Danieli, na kwa nini?
12 Upesi Danieli akapata kujua juu ya sheria hiyo iliyokataza kutoa sala. Mara moja, akaingia nyumbani mwake na kwenda kwenye chumba cha paa, ambapo madirisha yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu.b Huko, Danieli akaanza kusali kwa Mungu “kama ilivyokuwa kawaida yake.” (BHN) Huenda Danieli alifikiri alikuwa peke yake, lakini waliompangia njama walikuwa wakimtazama. Ghafula,“waliingia ndani,” yamkini kwa njia ileile walivyokusanyika kwa rabsharabsha walipomwendea Dario. Sasa walikuwa wakiona kwa macho yao wenyewe—Danieli alikuwa “akiomba dua na kumsihi Mungu wake.” (Danieli 6:10, 11, BHN) Mawaziri na maliwali walikuwa na uthibitisho wote waliouhitaji wa kumshtaki Danieli mbele ya mfalme.
13. Adui za Danieli waliripoti nini kwa mfalme?
13 Adui za Danieli walimwuliza Dario kwa hila: “Je! hukuitia sahihi ile marufuku, ya kwamba kila mtu atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme, atatupwa katika tundu la simba?” Dario akajibu, akasema: “Neno hili ni kweli, kama ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi isiyoweza kubadilika.” Sasa wapanga-njama hao wakasema mambo waziwazi. “Yule Danieli, aliye mmoja wa wana wa wale waliohamishwa wa Yuda, hakujali wewe, Ee mfalme, wala ile marufuku uliyoitia sahihi, bali aomba dua mara tatu kila siku.”—Danieli 6:12, 13.
14. Yaonekana ni kwa nini mawaziri na maliwali walimrejezea Danieli kuwa “mmoja wa wana wa wale waliohamishwa wa Yuda”?
14 Ni jambo lenye kutokeza kwamba mawaziri na maliwali walimrejezea Danieli kuwa “mmoja wa wana wa wale waliohamishwa wa Yuda.” Yaonekana kwamba walitaka kukazia kwamba Danieli ambaye Dario alikuwa amemkweza na kumpa umaarufu hivyo kwa hakika hakuwa mtu wa maana ila mtumwa Myahudi tu. Waliamini kwamba kwa sababu hiyo, alikuwa chini ya sheria—hata iwe mfalme alihisi namna gani juu yake!
-
-
Aokolewa Asiliwe na Simba!Sikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
12. (a) Danieli alifanya nini mara tu alipopata kujua juu ya sheria hiyo mpya? (b) Ni nani waliokuwa wakimtazama Danieli, na kwa nini?
12 Upesi Danieli akapata kujua juu ya sheria hiyo iliyokataza kutoa sala. Mara moja, akaingia nyumbani mwake na kwenda kwenye chumba cha paa, ambapo madirisha yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu.b Huko, Danieli akaanza kusali kwa Mungu “kama ilivyokuwa kawaida yake.”
-
-
Aokolewa Asiliwe na Simba!Sikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
b Chumba cha paa kilikuwa chumba cha faragha ambacho mtu angeweza kwenda ikiwa hakutaka kusumbuliwa.
-