-
Epafrasi—“Mhudumu Mwaminifu wa Kristo”Mnara wa Mlinzi—1997 | Mei 15
-
-
Mwanamume Aliyethamini Sala
Katika umalizio wa barua aliyotuma kwa Wakristo Wakolosai, Paulo asema hivi: “Epafrasi, ambaye ni kutoka miongoni mwenu, mtumwa wa Kristo Yesu, awapelekea nyinyi salamu zake, akijikakamua mwenyewe sikuzote kwa ajili yenu katika sala zake, ili nyinyi mwishowe mpate kusimama mkiwa kamili na kwa usadikisho imara katika mapenzi yote ya Mungu. Kwa kweli namtolea yeye ushahidi kwamba hujitahidi sana mwenyewe kwa niaba yenu na ya wale walio Laodikia na ya wale walio Hierapolisi.”—Wakolosai 4:12, 13.
Ndiyo, hata alipokuwa ‘mateka mwenzake’ Paulo katika Roma, Epafrasi alikuwa akifikiria ndugu zake wapendwa katika Kolosai, Laodikia, na Hierapolisi na kusali kwa ajili yao. (Filemoni 23) Kwa jinsi ilivyo, ‘alijikakamua’ kwa ajili yao katika sala. Kulingana na msomi D. Edmond Hiebert, neno la Kigiriki litumikalo hapa hudokeza “utendaji wa kujitahidi na wa kujidhabihu sana,” jambo lifananalo na “maumivu makali” ya akilini yaliyompata Yesu Kristo aliposali katika bustani ya Gethsemane. (Luka 22:44) Epafrasi alitamani kwa moyo kwamba ndugu na dada zake wa kiroho wafikie uthabiti na ukomavu kamili wa Kikristo. Lazima ndugu huyo mwenye akili ya kiroho awe alikuwa baraka kama nini kwa makutaniko!
-
-
Epafrasi—“Mhudumu Mwaminifu wa Kristo”Mnara wa Mlinzi—1997 | Mei 15
-
-
Kusali kwa ajili ya wengine, kama alivyofanya Epafrasi, ni aina ya utumishi mtakatifu ambayo wote wanaweza kufanya. Huenda sala hizo zikahusisha maneno ya hangaiko kwa ajili ya waabudu wa Yehova wanaolazimika kukabili hatari au magumu mbalimbali ya kiroho au kimwili. Kwa kujikakamua wenyewe kwa nguvu hivyo, twaweza kuwa kama Epafrasi. Kila mmoja wetu aweza kuwa na pendeleo na shangwe ya kujithibitisha kuwa ‘mtumwa mwenzi mpendwa’ katika familia ya watumishi waaminifu wa Yehova.
-