Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Hana Alivyopata Amani
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Machi 15
    • Hana Anaweka Nadhiri

      Dhabihu za ushirika zililiwa katika patakatifu pa Yehova. Baada ya kuondoka katika chumba cha kulia chakula, Hana anasali kwa Mungu. (1 Samweli 1:9, 10) “Ee Yehova wa majeshi,” Hana anasihi, “ikiwa hakika utayaona mateso ya kijakazi wako, nawe kwa kweli unikumbuke, na ikiwa hutamsahau kijakazi wako na kwa kweli umpe kijakazi wako uzao wa kiume, mimi nitamtoa kwa Yehova siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita juu ya kichwa chake.”—1 Samweli 1:11.

      Hana anataja mambo hususa katika sala. Anaomba mtoto wa kiume na kuweka nadhiri kwamba mtoto huyo atawekwa wakfu kwa Yehova na kuwa Mnadhiri maisha yake yote. (Hesabu 6:1-5) Nadhiri kama hiyo inategemea kibali cha mume wake, na mambo ambayo Elkana anafanya baadaye yanaonyesha kwamba anakubali ahadi ya mke wake mpendwa.—Hesabu 30:6-8.

      Hana anatoa sala kwa njia ambayo inamfanya Kuhani Mkuu Eli afikiri kwamba Hana amelewa. Midomo yake inatetemeka, lakini Eli hasikii sauti yoyote, kwa kuwa Hana anasali moyoni mwake. Anasali kwa bidii sana. (1 Samweli 1:12-14) Wazia jinsi Hana anavyohisi Eli anapomshtumu kwamba amelewa! Hata hivyo, anamjibu kuhani huyo mkuu kwa heshima. Eli anapotambua kwamba Hana amekuwa akisali “kutokana na wingi wa mahangaiko [yake] na usumbufu [wake],” anasema: “Mungu wa Israeli akupe ombi lako.” (1 Samweli 1:15-17) Baada ya hapo, Hana anaenda zake na kula chakula, na ‘uso wake hauonyeshi tena kuhangaika.’—1 Samweli 1:18.

      Tunaweza kujifunza nini kutokana na mambo hayo yote? Tunaposali kwa Yehova kuhusu mahangaiko yetu, tunaweza kumwambia jinsi tunavyohisi na kusali kutoka moyoni kuhusu kile tunachotaka. Ikiwa hatuwezi kufanya jambo lingine lolote ili kutatua tatizo hilo, tunapaswa kuacha mambo mikononi mwake. Hakuna njia iliyo bora kuliko hiyo.—Methali 3:5, 6.

      Baada ya kusali kwa bidii, inaelekea sana kwamba watumishi wa Yehova watakuwa na amani kama ile ya Hana. Mtume Paulo aliandika hivi kuhusu sala: “Msihangaike juu ya kitu chochote, bali katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote itailinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kwa njia ya Kristo Yesu.” (Wafilipi 4:6, 7) Tunapomtupia Yehova mzigo wetu, tunapaswa kumwachia ili auchukue. Kisha, kama Hana, hatuhitaji kuendelea kuhangaika.—Zaburi 55:22.

  • Jinsi Hana Alivyopata Amani
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Machi 15
    • Sala Yenye Shangwe ya Hana

      Sasa Hana ambaye hapo awali alikuwa tasa, ni mwenye shangwe iliyoje! Ni sala chache zilizotolewa na wanawake ambazo zimeandikwa katika Maandiko. Hata hivyo, tunajulishwa kuhusu sala mbili ambazo Hana alitoa. Ya kwanza inahusu hisia zake aliposumbuliwa na kuteswa, na ya pili ni sala ya shukrani yenye furaha. Hana anaanza hivi: “Moyo wangu unafurahi katika Yehova.” Anashangilia kwamba “hata aliye tasa amezaa,” na anamtukuza Yehova kuwa “Mwenye Kuinua mtu wa hali ya chini kutoka mavumbini.” Kwa kweli, “humwinua maskini kutoka katika shimo la majivu.”—1 Samweli 2:1-10.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki