-
Jinsi ya Kumkaribia “Msikiaji wa Sala”Mnara wa Mlinzi—2006 | Septemba 1
-
-
Mzee huyo mwaminifu alimuuliza Yehova kuhusu mrithi, akisema: “Utanipa nini, kwa sababu mimi naenda zangu bila mtoto?” (Mwanzo 15:2, 3; 17:18) Pindi nyingine, Abrahamu alitaka kujua ikiwa watu fulani wangeokolewa wakati ambapo Mungu angeleta hukumu dhidi ya waovu waliokuwa huko Sodoma na Gomora. (Mwanzo 18:23-33) Isitoshe, Abrahamu aliomba dua kwa ajili ya watu wengine. (Mwanzo 20:7, 17)
-
-
Jinsi ya Kumkaribia “Msikiaji wa Sala”Mnara wa Mlinzi—2006 | Septemba 1
-
-
7. Wazee wa ukoo walisali kwa Yehova kuhusu mambo gani?
7 Wazee wa ukoo walisali kuhusu mambo mbalimbali, na Yehova aliwasikia. Yakobo aliweka nadhiri kupitia sala. Baada ya kumwomba Mungu amtegemeze, Yakobo alitoa ahadi hii nzito: “Katika kila kitu utakachonipa bila shaka nitakupa wewe sehemu ya kumi.” (Mwanzo 28:20-22) Baadaye, alipokuwa karibu kukutana na ndugu yake, Yakobo alimsihi sana Yehova amlinde, akisema: “Nakuomba, unikomboe kutoka katika mkono wa ndugu yangu, kutoka katika mkono wa Esau, kwa sababu mimi ninaogopa.” (Mwanzo 32:9-12) Yule mzee wa ukoo Ayubu alisali kwa Yehova kwa niaba ya familia yake, huku akitoa dhabihu kwa ajili yao. Wakati marafiki watatu wa Ayubu walipotenda dhambi kwa kusema mambo yasiyofaa, Ayubu alisali kwa ajili yao, naye “Yehova akaukubali uso wa Ayubu.” (Ayubu 1:5; 42:7-9) Masimulizi hayo yanatusaidia kutambua mambo tunayoweza kutaja tunaposali kwa Yehova.
-