-
Mikutano Kwa Ajili ya Ibada, Funzo, na Kitia-moyoMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Ndugu Russell aling’amua kwamba mengi yalihitajiwa zaidi ya kujifunza mambo ya kimafundisho tu. Lazima kuwe pia na wonyesho wa ujitoaji ili mioyo ya watu isukumwe na uthamini wa upendo wa Mungu na tamaa ya kumheshimu na kumtumikia. Madarasa yalihimizwa yapange mkutano wa pekee kwa kusudi hilo mara moja kila juma. Ilirejezewa nyakati nyingine kuwa “Mikutano ya Nyumbani” kwa sababu ilifanywa katika makao ya watu binafsi. Programu ilitia ndani sala, nyimbo za sifa, na shuhuda zilizosimuliwa na wale waliohudhuria.b Shuhuda hizo zilikuwa nyakati nyingine mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo; majaribu, magumu, na matatizo yaliyokabiliwa wakati wa siku za karibuni yalitiwa ndani pia.
-
-
Mikutano Kwa Ajili ya Ibada, Funzo, na Kitia-moyoMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
b Kwa sababu ya yale yaliyoandikwa, mikutano hiyo iliitwa pia Mikutano ya Sala, Sifa na Ushuhuda. Kwa sababu ya umaana wa sala, baada ya wakati ilipendekezwa kwamba mara moja kila miezi mitatu mkutano uwe ibada ya sala tu, kutia na nyimbo lakini bila yaliyoonwa.
-