-
Je, Mungu Ana Watu Wanaomtumikia kwa Utaratibu?Mnara wa Mlinzi—2011 | Juni 1
-
-
▪ Wakristo wa kweli wamepangwa kwa utaratibu ili kutimiza kazi fulani. (Mathayo 24:14; 1 Timotheo 2:3, 4) Yesu aliwaamuru wafuasi wake wahubiri habari njema za Ufalme kwa mataifa yote, kazi ambayo haingewezekana bila kuwa na watu kutoka katika mataifa yote ambao wanaifanya kwa utaratibu na kwa umoja. Kwa mfano, unaweza kumlisha mtu mmoja peke yako, lakini kama ingekupasa kulisha maelfu ya watu, hata mamilioni, ungehitaji kikundi cha watu chenye utaratibu mzuri na kinachofanya kazi kwa ushirikiano. Ili kutimiza kazi yao, Wakristo wa kweli wanatumikia “bega kwa bega,” au “kwa moyo mmoja.” (Sefania 3:9; BHN) Je, ingewezekana kufanya kazi inayohusisha mataifa, lugha, na jamii mbalimbali bila kuwa na watu wenye utaratibu na umoja? Jibu ni wazi.
-
-
Je, Mungu Ana Watu Wanaomtumikia kwa Utaratibu?Mnara wa Mlinzi—2011 | Juni 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 14, 15]
Utaratibu unahitajiwa ili kuhubiri katika mataifa yote
Kuhubiri nyumba kwa nyumba
Kutoa misaada wakati wa msiba
Makusanyiko
Ujenzi wa majengo ya ibada
-