Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka
    Huduma ya Ufalme—1997 | Februari
    • 2 Unaweza kuanza mazungumzo kwa kutaja kifupi baadhi ya matatizo yanayokabiliwa katika jumuiya, kisha uweze kusema:

      ◼ “Watu wengi huamini kwamba kuna Mungu, lakini wanajiuliza: ‘Ni wakati ujao wa aina gani anaotutakia?’ Ungejibuje hilo? [Ruhusu itikio.] Je, ulijua kwamba Biblia hueleza waziwazi mapenzi ya Mungu kwa wanadamu na hatua anazochukua kuyatimiza?” Fungua ukurasa wa 301 katika kitabu Upeo wa Ufunuo. Soma Ufunuo 21:1 katika fungu la 1, kisha usome maelezo yanayotolewa kulihusu katika nusu ya mwisho wa fungu la 2. Fungua picha kwenye ukurasa 302 uonyeshe kinachomaanishwa kwa wakati wetu ujao. Soma Ufunuo 21:4 katika fungu la 6. Ikiwa kuna itikio zuri, toa kitabu. Panga wakati unaofaa wa kurudi ili kuendeleza mazungumzo.

  • Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka
    Huduma ya Ufalme—1997 | Februari
    • 4 Kwa kuwa wengi wanahangaishwa na matatizo yenye kuongezeka yanayokabili wanadamu, unaweza kusema jambo kama hili katika ziara yako ya kwanza:

      ◼ “Karibu kila mtu ninayekutana naye anahangaishwa na matatizo tunayokabili katika jumuiya yetu. [Taja machache.] Kwa miongo kadhaa wanadamu wameahidi kuleta matatuzi ya daima, na wengine wamejaribu kufanya hivyo. Unafikiri ni nini ambacho husababisha hali ziendelee kuwa mbaya zaidi? [Ruhusu itikio.] Biblia hutoa elezo ambalo watu walio wengi hawajapata kamwe kulifikiria. Kitabu cha Ufunuo hufafanua vita iliyotokea mbinguni. Ona tokeo, kama inavyosemwa kwenye Ufunuo 12:9.” Soma mstari huo, kisha ufungue ukurasa wa 182 katika kitabu Upeo wa Ufunuo. Tumia picha ueleze kujihusisha kwa Shetani katika mambo ya duniani. Toa kitabu kwa mchango wa kawaida. Fanya mipango ya kurudi uzungumzie jinsi Mungu atakavyotatua matatizo ya wanadamu.

  • Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka
    Huduma ya Ufalme—1997 | Februari
    • 6 Kukiwa na watu wengi wenye kupendezwa na mazingira, unaweza kusema jambo kama hili ili kuanzisha mazungumzo:

      ◼ “Tumeona kwamba karibu kila mtu anahangaikia uchafuzi wa hewa, maji, na chakula. Katika nchi kadhaa hali ya mazingira tayari inatishia uhai. Kwa kuwa Mungu ndiye Muumba wa dunia, unafikiri atafanya nini kuhusu hilo? [Ruhusu itikio.] Biblia husema kwamba Mungu atatoza hesabu kuhusu jinsi tunavyoitumia dunia. [Soma Ufunuo 11:18b.] Wazia kuishi kwenye dunia ambayo haina uchafuzi!” Eleza juu ya ahadi ya Mungu ya paradiso, kama inavyoonyeshwa kwenye Ufunuo 21:3, 4. Onyesha picha iliyo kwenye ukurasa wa 302 katika kitabu Upeo wa Ufunuo. Ikiwa kuna kupendezwa, toa kitabu na upange kurudi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki