-
Yehova Huchukia Mwenendo wa HilaMnara wa Mlinzi—2002 | Mei 1
-
-
Mstari wa 7 unaonyesha jambo moja lililo wazi: “Yapasa midomo ya kuhani ihifadhi maarifa, tena yawapasa watu kuitafuta sheria kinywani mwake; kwa kuwa yeye ni mjumbe wa BWANA wa majeshi.” Zaidi ya miaka elfu moja mapema, sheria za Mungu ambazo Waisraeli walipewa kupitia Musa zilisema kwamba makuhani walikuwa na daraka la ‘kuwafundisha wana wa Israeli amri zote ambazo Yehova aliwaambia.’ (Mambo ya Walawi 10:11) Kwa kusikitisha, baadaye mwandishi wa 2 Mambo ya Nyakati 15:3 aliripoti hivi: “Tangu siku nyingi Israeli wamekuwa hawana Mungu wa kweli, wala hawana kuhani afundishaye, wala hawana torati.”
-
-
Yehova Huchukia Mwenendo wa HilaMnara wa Mlinzi—2002 | Mei 1
-
-
Huenda ikawa makuhani fulani wa wakati huo walitimiza viwango vya Mungu, na kuna kuhani mmoja aliyevitimiza baadaye. Huyo alikuwa Yesu, “kuhani wa cheo cha juu.” (Waebrania 3:1) Kwa kweli, ingeweza kusemwa hivi kumhusu: “Sheria ya kweli ilikuwa kinywani mwake, wala udhalimu haukuonekana midomoni mwake; alikwenda pamoja nami katika amani na unyofu, na kuwageuza wengi hata wakaacha uovu.”—Malaki 2:6.
9. Ni nani wanaoandaa kwa uaminifu kweli za Biblia wakati wetu?
9 Hali kadhalika, kwa muda unaozidi karne moja sasa, ndugu watiwa-mafuta wa Kristo ambao wana tumaini la kuishi mbinguni, wametumikia wakiwa “ukuhani mtakatifu, ili kutoa dhabihu za kiroho zenye kukubalika kwa Mungu.” (1 Petro 2:5) Wanaongoza katika kuandalia wengine kweli za Biblia. Wewe mwenyewe umejionea kutokana na kweli ambazo wanafundisha kwamba sheria ya kweli iko kinywani mwao. Sivyo? Wamesaidia wengi waache mafundisho ya dini isiyo ya kweli, na sasa kuna mamilioni ya watu ulimwenguni pote ambao wamejifunza kweli za Biblia na ambao wana tumaini la kuishi milele. Watu hao nao wana pendeleo la kufundisha mamilioni ya wengine sheria ya kweli.—Yohana 10:16; Ufunuo 7:9.
-