-
Yehova ni Mungu wa MaaganoMnara wa Mlinzi—1998 | Februari 1
-
-
9. (a) Yehova aliahidi mambo gani manne kupitia agano la Kiabrahamu? (b) Ni matazamio gani zaidi yaliyowezeshwa na agano la Yehova pamoja na Israeli, na kwa masharti gani?
9 Yehova alieleza Israeli masharti ya agano hilo kwa kusema: “Ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila yote ya watu; maana dunia yote pia ni mali yangu, nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu.” (Kutoka 19:5, 6) Yehova alikuwa ameahidi kwamba mbegu ya Abrahamu (1) ingepata kuwa taifa kubwa, (2) ingepewa ushindi dhidi ya adui zake, (3) ingerithi nchi ya Kanaani, na (4) ingekuwa njia ambayo kwayo mataifa yangebarikiwa. Sasa alifunua kwamba ikiwa wangezitii amri zake, wao wenyewe wangeweza kurithi baraka hizo wakiwa watu wake wa pekee, Israeli, “ufalme wa makuhani, na taifa takatifu.” Je, Waisraeli walikubali kuingia katika agano hilo? Walijibu kwa umoja hivi: “Hayo yote aliyoyasema BWANA tutayatenda.”—Kutoka 19:8.
-
-
Yehova ni Mungu wa MaaganoMnara wa Mlinzi—1998 | Februari 1
-
-
12 Je, Israeli lilipata kuwa “ufalme wa makuhani”? Tangu mwanzo kabisa, lilikuwa ufalme, Yehova akiwa Mfalme wa kimbingu. (Isaya 33:22) Zaidi, agano la Sheria lilitia ndani maandalizi kwa ajili ya umaliki wa kibinadamu, hivi kwamba baadaye Yehova aliwakilishwa na wafalme waliotawala huko Yerusalemu. (Kumbukumbu la Torati 17:14-18) Lakini, je, Israeli lilikuwa ufalme wa makuhani? Lilikuwa na ukuhani uliotoa utumishi mtakatifu kwenye tabenakulo. Lile tabenakulo (baadaye, hekalu) lilikuwa kitovu cha ibada safi kwa ajili ya Waisraeli na pia kwa ajili ya wasio Waisraeli. Nalo taifa lilikuwa njia ya pekee ya kupata kweli iliyofunuliwa kwa wanadamu. (2 Mambo ya Nyakati 6:32, 33; Waroma 3:1, 2) Waisraeli wote waaminifu, wala si makuhani wa Kilawi tu, walikuwa “mashahidi” wa Yehova. Israeli lilikuwa “mtumishi,” wa Yehova aliyefanyizwa ili ‘azitangaze sifa zake.’ (Isaya 43:10, 21) Wageni wengi wanyenyekevu waliona nguvu za Yehova kwa niaba ya watu wake na kuvutiwa na ibada safi. Wakapata kuwa wageuzwa-imani. (Yoshua 2:9-13) Lakini kabila moja tu ndilo kwa kweli lililotumikia likiwa makuhani watiwa-mafuta.
-