-
‘Weka Moyoni Mwako’ Hekalu la Mungu!Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
-
-
Na zaidi, makuhani katika ono hilo hufananisha jamii ya kikuhani ya watiwa-mafuta wakiwa wangali duniani, wala si baada ya ufufuo wao wa kimbingu au wakati wa kipindi cha Milenia. Kwa nini? Ona kwamba makuhani hao wanaonyeshwa wakitumikia katika ua wa ndani. Makala katika Mnara wa Mlinzi yameonyesha kwamba ua huo hufananisha ule msimamo wa kipekee ambao makuhani wa cheo cha chini wa Kristo wanao wakiwa wangali duniani.c Pia ona kwamba ono hilo hukazia kutokamilika kwa makuhani hao. Wanaambiwa watoe dhabihu kwa ajili ya dhambi zao wenyewe. Wanaonywa juu ya hatari ya kuwa wachafu—kiroho na kiadili. Kwa hivyo, hawafananishi wale watiwa-mafuta waliofufuliwa, ambao mtume Paulo aliandika hivi kuwahusu: “Tarumbeta itavuma, na wafu watafufuliwa wakiwa wasioharibika.” (1 Wakorintho 15:52; Ezekieli 44:21, 22, 25, 27) Makuhani katika ono hilo huchangamana na kutumikia watu moja kwa moja. Haitakuwa hivyo katika Paradiso, wakati jamii ya kikuhani itakuwa mbinguni. Kwa hiyo, ono hilo hutoa mfano bora kabisa wa jinsi ambavyo watiwa-mafuta hufanya kazi kwa ukaribu na “umati mkubwa” ulio duniani leo.—Ufunuo 7:9; Ezekieli 42:14.
-
-
Lile “Hekalu” na Yule “Mkuu” LeoMnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
-
-
Ukuhani Mwaminifu
9, 10. “Ukuhani wa kifalme,” kama ulivyotangulia kuonyeshwa na jamii ya kikuhani katika ono la Ezekieli, umetoa ufundishaji wa kiroho jinsi gani?
9 Katika nyakati za kabla ya Ukristo, makuhani walifanya kazi ngumu hekaluni. Kazi ya kuchinja wanyama wa dhabihu, kuwatoa kwenye madhabahu, na kuwatumikia makuhani wenzao na watu ilikuwa yenye kuchosha sana. Lakini walikuwa na kazi nyingine muhimu. Yehova aliamuru hivi kuhusu makuhani hao: “Watawafundisha watu wangu tofauti iliyopo kati ya vitu vitakatifu na vitu vya sikuzote [“vichafu,” NW], na kuwafundisha kupambanua kati ya yaliyo machafu na yaliyo safi.”—Ezekieli 44:23; Malaki 2:7.
10 Je, unathamini kazi ngumu na utumishi mnyenyekevu ambao watiwa-mafuta wakiwa kikundi, “ukuhani wa kifalme,” wamefanya kwa ajili ya ibada safi? (1 Petro 2:9) Kama ukuhani wa Kilawi wa zamani, wameongoza katika kutoa mafundisho ya kiroho, wakisaidia watu kuelewa kile ambacho ni safi na chenye kukubalika machoni pa Mungu na kile ambacho si safi na kisichokubalika. (Mathayo 24:45) Mafundisho hayo, yanayotolewa kupitia vichapo vinavyotegemea Biblia na mikutano ya Kikristo na mikusanyiko, yamewasaidia mamilioni ya watu kupatanishwa na Mungu.—2 Wakorintho 5:20.
11. (a) Ono la Ezekieli lilikaziaje umuhimu wa usafi kwa makuhani? (b) Katika siku za mwisho, watiwa-mafuta wamesafishwaje katika maana ya kiroho?
11 Hata hivyo, ni lazima makuhani wafanye mengi zaidi ya kufundisha wengine wawe safi; ni lazima wao wenyewe wawe safi. Hivyo basi, Ezekieli aliona kimbele hatua ya kusafishwa kwa ukuhani wa Israeli. (Ezekieli 44:10-16) Vivyo hivyo, historia yaonyesha kwamba mwaka wa 1918, Yehova aliketi “kama asafishaye” katika hekalu lake la kiroho, akiichunguza jamii ya kikuhani ya watiwa-mafuta. (Malaki 3:1-5) Wale walioonwa kuwa safi kiroho au waliotubu kuhusu ibada yao ya sanamu ya hapo awali, waliruhusiwa kuendelea na pendeleo la utumishi katika hekalu lake la kiroho. Na bado, sawa na watu wale wengine wote, watiwa-mafuta wakiwa mtu mmoja-mmoja wanaweza kuwa wachafu—kiroho na kiadili. (Ezekieli 44:22, 25-27) Imewalazimu kujitahidi sana ili kubaki “bila doa kutokana na ulimwengu.”—Yakobo 1:27; linganisha Marko 7:20-23.
12. Kwa nini twapaswa kuthamini kazi ya watiwa-mafuta?
12 Kila mmoja wetu aweza kujiuliza, ‘Je, ninathamini kielelezo kilichowekwa na watiwa-mafuta kwa miaka mingi ya utumishi wao mwaminifu? Je, ninaiga imani yao?’ Ni vizuri kwa wale wa umati mkubwa kukumbuka kwamba hawatakuwa na watiwa-mafuta sikuzote hapa duniani. Yehova alisema hivi kuhusu makuhani katika ono la Ezekieli: “Wala hamtawapa milki [ya nchi] iwayo yote katika Israeli; mimi ni milki yao.” (Ezekieli 44:28) Vivyo hivyo, watiwa-mafuta hawana sehemu yoyote yenye kudumu milele hapa duniani. Wao wana urithi wa kimbingu, na wale wa umati mkubwa huliona kuwa pendeleo kuwaunga mkono na kuwatia moyo wakiwa wangali hapa duniani.—Mathayo 25:34-40; 1 Petro 1:3, 4.
-
-
Lile “Hekalu” na Yule “Mkuu” LeoMnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
-
-
15. (a) Ono la Ezekieli hutufafanuliaje uhusiano uliopo baina ya wazee ambao ni wa umati mkubwa na jamii ya kikuhani ya watiwa-mafuta? (b) Wazee watiwa-mafuta wamechukua uongozi upi katika tengenezo la Mungu la kidunia?
15 Lakini je, ni uhusiano gani uliopo baina ya jamii ya kikuhani ya watiwa-mafuta na wanaume wazee hao ambao, wakiwa sehemu ya umati mkubwa, wanatumikia katika vyeo vya usimamizi? Ono la Ezekieli ladokeza kwamba fungu la wazee hao walio washiriki wa umati mkubwa ni la chini na la kuunga mkono, huku watiwa-mafuta wakichukua uongozi wa kiroho. Jinsi gani? Kumbuka, makuhani katika ono hilo walipewa daraka la kufundisha watu mambo ya kiroho. Pia waliambiwa watumikie wakiwa mahakimu katika kesi za kisheria. Kwa kuongezea, Walawi walipewa kazi ya kuwa “wasimamizi” katika malango ya hekalu. (Ezekieli 44:11, 23, 24) Kwa wazi, mkuu huyo alipaswa kujitiisha kwa utumishi wa kiroho na uongozi wa hao makuhani. Basi, inafaa kwamba katika nyakati za kisasa watiwa-mafuta wamechukua uongozi katika ibada safi. Kwa mfano, washiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova wamechaguliwa kutoka miongoni mwao. Wazee hao waaminifu, watiwa-mafuta, wamekuwa wakiizoeza kwa makumi ya miaka jamii ya mkuu huyo inayokua. Washiriki hao wa Baraza Linaloongoza wanawatayarisha wale wanaotazamia kuwa washiriki wa jamii hii kwa ajili ya siku watakapoachiwa mamlaka kamili ya madaraka yao katika ulimwengu mpya wa Mungu unaokuja.
-