-
Uzuri Mwingi Mno wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha KimbinguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Kutambulisha Wale Wazee 24
8. Ni nani ambao Yohana anaona kuzunguka kiti cha ufalme cha Yehova, na hao wanawakilisha nani?
8 Yohana alijua kwamba makuhani waliwekwa rasmi watumikie katika ile tabenakulo ya kale. Kwa hiyo huenda akawa alishangaa alipoona anachofuata kueleza: “Na kuzunguka kiti cha ufalme kuna viti vya ufalme ishirini na vinne, na juu ya viti vya ufalme hivi mimi niliona wameketi wazee ishirini na wanne wamevalia mavazi ya nje meupe, na juu ya vichwa vyao mataji ya dhahabu.” (Ufunuo 4:4, NW) Ndiyo, badala ya makuhani, kuna wazee 24, wameketishwa katika viti vya ufalme na kuvikwa mataji kama wafalme. Wazee hawa ni akina nani? Wao si wengine ila wapakwa-mafuta wa kundi la Kikristo, wamefufuliwa na kuchukua cheo cha kimbingu ambacho Yehova aliwaahidi.
-
-
Uzuri Mwingi Mno wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha KimbinguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Lakini mgawo wa kimbingu wa hawa wazee 24 si wa utawala wa kiserikali tu. Katika utangulizi wa kitabu cha Ufunuo, Yohana alisema hivi kwa habari ya Yesu: “Yeye alifanya sisi kuwa ufalme, makuhani kwa Mungu na Baba yake.” (Ufunuo 1:5, 6, NW) Hawa ni wafalme na makuhani pia. “Wao watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, na watatawala wakiwa wafalme pamoja na yeye kwa miaka elfu.”—Ufunuo 20:6, NW.
11. Ni kwa nini inafaa kwamba nambari ya wale wazee ni 24, na nambari hiyo inamaanisha nini?
11 Ni nini lililo la maana kwa habari ya nambari 24, kwa kuwa Yohana anaona wazee 24 kuzunguka kiti cha ufalme? Katika njia nyingi, hawa walitangulia kufananishwa na wale makuhani waaminifu wa Israeli wa kale. Mtume Petro aliandikia Wakristo wapakwa-mafuta hivi: “Nyinyi ni ‘jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu kwa ajili ya mali ya pekee.’” (1 Petro 2:9, NW) Kwa kupendeza, ukuhani huo wa kale wa Kiyahudi, ulikuja kugawanywa ukawa migawanyo 24. Kila mgawanyo ulipewa mgawo wa majuma yao wenyewe katika mwaka wa kutumikia mbele za Yehova, hivi kwamba utumishi mtakatifu ulitolewa bila kukatizwa. (1 Nyakati 24:5-19) Basi, inafaa kwamba wako wazee 24 wakionyeshwa katika njozi ya Yohana ya ule ukuhani wa kimbingu kwa sababu huu ukuhani unatumikia Yehova kwa kuendelea, bila kukoma. Utakapokamilishwa, itakuwako migawanyo 24, kila mmoja ukiwa na washindi 6,000, kwa kuwa Ufunuo 14:1-4 hutuambia kwamba 144,000 (24 x 6,000) ‘wananunuliwa miongoni mwa aina ya binadamu’ wakasimame juu ya Mlima Sayuni wa kimbingu pamoja na Mwana-Kondoo, Yesu Kristo. Kwa kuwa nambari 12 huashiria tengenezo la kimungu lenye usawaziko, 24 hurudufisha—au huimarisha—mpango kama huo.
-