-
Christophe Plantin Mtangulizi wa Uchapishaji wa BibliaMnara wa Mlinzi—2006 | Novemba 15
-
-
“Kazi Muhimu Zaidi ya Uchapishaji”
Mnamo mwaka wa 1567, upinzani kwa utawala wa Hispania ulipokuwa ukiongezeka katika Nchi za Chini, Mfalme Philip wa Pili wa Hispania alimtuma Mtawala wa jimbo la Alba ili awe gavana huko. Akiwa na mamlaka kamili aliyopewa na mfalme, mtawala huyo alijaribu kukomesha upinzani wa Waprotestanti uliokuwa ukiongezeka. Kwa hiyo, Plantin alianzisha mradi mkubwa ambao alitumaini ungewafanya watu waache kumshuku kuwa mwasi wa kidini. Alitamani sana kuchapisha tafsiri ya wasomi ya maandishi ya Biblia katika lugha za awali. Ili kuichapisha, Plantin alifaulu kupata msaada wa Philip wa Pili. Mfalme huyo aliahidi kumpa msaada wa kifedha na kumtuma mteteaji maarufu wa haki za kibinadamu Arias Montano ili asimamie mradi huo.
Montano alikuwa na kipawa cha lugha, naye alifanya kazi kwa saa 11 kila siku. Alisaidiwa na wataalamu wa lugha wa Hispania, Ubelgiji, na Ufaransa. Kusudi lao lilikuwa kutayarisha tafsiri mpya ya Biblia maarufu ya Complutensian Polyglot.b Mbali na Vulgate ya Kilatini, Septuajinti ya Kigiriki, na maandishi ya awali ya Kiebrania, Biblia mpya ya Polyglot ya Plantin ilikuwa na Targumi ya Kiaramu, Peshitta ya Kisiria, na tafsiri nyingine za Kilatini za neno kwa neno zinazotambuliwa.
Kazi ya uchapishaji ilianza mwaka wa 1568. Kazi hiyo kubwa ilifanywa haraka sana na kukamilishwa mwaka wa 1572. Montano alisema hivi katika barua aliyomwandikia Mfalme Philip wa Pili: “Kazi kubwa inafanywa hapa kwa mwezi mmoja kuliko ile inayofanywa Roma kwa mwaka mmoja.” Plantin alichapisha nakala 1,213 za Biblia mpya ya Polyglot. Kila nakala ilikuwa na mabuku manane makubwa. Kwenye ukurasa wa kwanza wa Biblia hiyo, kulikuwa na picha ya simba, ng’ombe-dume, mbwa-mwitu, na mwana-kondoo wakila pamoja kwa amani katika chombo kimoja, kama inavyoonyeshwa katika Isaya 65:25. Bei ya mabuku ambayo hayakuwa yameunganishwa ilikuwa gilda 70 (pesa za Uholanzi). Ilikuwa bei ghali kwa sababu wakati huo familia ya kawaida ilipata mshahara wa gilda 50 hivi kwa mwaka. Baadaye, Biblia yenye jalada iliitwa Antwerp Polyglot. Pia, iliitwa Biblia Regia (Biblia ya Kifalme) kwa sababu Mfalme Philip wa Pili ndiye aliyeutegemeza kifedha mradi huo.
Hata ingawa Papa Gregory wa 13 alikubali Biblia hiyo, Arias Montano alishutumiwa vikali kwa sababu ya kazi yake. Sababu moja ni kwamba Montano aliona maandishi ya awali ya Kiebrania kuwa bora kuliko Vulgate ya Kilatini. Mpinzani wake mkuu alikuwa León de Castro, mwanatheolojia Mhispania ambaye aliiona Vulgate ya Kilatini kuwa yenye mamlaka kamili. De Castro alimshutumu Montano kwamba aliivuruga Biblia kwa kuingiza falsafa zinazopinga Utatu. Kwa mfano, de Castro alidai kwamba Peshitta ya Kisiria haikuwa na sehemu ifuatayo iliyoongezwa kwa uwongo kwenye andiko la 1 Yohana 5:7: “Mbinguni, Baba, Neno, na Roho Mtakatifu: na watatu hawa ni mmoja.” (King James Version) Hata hivyo, Baraza la Kihispania la Kuwahukumu Waasi wa Kidini, halikumpata Montano na hatia ya uasi. Tafsiri ya Antwerp Polyglot huonwa na watu fulani kuwa “kazi muhimu zaidi ya uchapishaji iliyofanywa na mchapishaji mmoja katika karne ya 16.”
-
-
Christophe Plantin Mtangulizi wa Uchapishaji wa BibliaMnara wa Mlinzi—2006 | Novemba 15
-
-
[Picha katika ukurasa wa 16]
Biblia ya “Antwerp Polyglot” ina maandishi ya Kiebrania, “Vulgate” ya Kilatini, “Septuajinti” ya Kigiriki, “Peshitta” ya Kisiria, na Targumi ya Kiaramu pamoja na tafsiri zake za Kilatini
[Picha zimeandalia na]
By courtesy of Museum Plantin-Moretus/Stedelijk Prentenkabinet Antwerpen
-