-
Yehova Huwapa Thawabu Kubwa Wale Wanaoishika Njia YakeMnara wa Mlinzi—2005 | Agosti 1
-
-
Punde tu baada ya kuachiliwa mwaka wa 1952, nilikutana na Nela, dada mmoja painia ambaye alikuwa mwenye bidii. Alikuwa akifanya upainia kusini mwa Poland. Baadaye, alifanya kazi mahali fulani pa siri ambapo tulipaita “kiwanda cha kuokea mikate,” mahali ambapo vichapo vyetu vilichapwa. Hiyo ilikuwa kazi ngumu ambayo ilihitaji tahadhari na kujitoa.
-
-
Yehova Huwapa Thawabu Kubwa Wale Wanaoishika Njia YakeMnara wa Mlinzi—2005 | Agosti 1
-
-
Kusimamia “Viwanda vya Kuokea Mikate”
Siku hizo, mwangalizi wa wilaya alisimamia “viwanda vya kuokea mikate,” vilivyokuwa mahali pa siri. Polisi walitufuata daima, huku wakijaribu kupata na kukomesha kazi yetu ya kuchapisha. Nyakati nyingine walifaulu, lakini hatukuwahi kukosa chakula cha kiroho kifaacho. Ilikuwa wazi kwamba Yehova alikuwa akitulinda.
Ili kualikwa kufanya kazi ngumu na hatari ya kuchapisha, ilihitaji mtu awe mshikamanifu, mwenye tahadhari, mwenye kujitoa, na mtiifu. Hizo ndizo sifa ambazo ziliwezesha “kiwanda cha kuokea mikate” kuendelea kufanya kazi kwa usalama. Ilikuwa vigumu kupata mahali pazuri pa kuchapisha kisiri. Sehemu fulani zilionekana kuwa zilizofaa, lakini akina ndugu waliokuwa katika sehemu hizo hawakuwa waangalifu sana. Katika sehemu nyingine, ingawa ndugu walikuwa waangalifu hali hazikufaa. Ndugu walikuwa tayari kujitoa. Niliwathamini sana ndugu na dada wote ambao nilikuwa na pendeleo la kufanya kazi nao.
-