-
Kutunza Mali za Bwana-MkubwaHuduma ya Ufalme—1998 | Juni
-
-
8 Hata iwe uchapaji uliongezeka kadiri gani Marekani, haukuwa mwingi vya kutosha kugawia ulimwengu wote. Kwa hiyo, miaka iliyofuata vita, utendaji wa uchapaji ulianzishwa au ulikuwa tayari ukiendelea katika nchi nyingi, kutia ndani Afrika Kusini, Denmark, Kanada, Ugiriki, Uingereza, Ujerumani Magharibi, na Uswisi. Kufikia miaka ya mapema ya 1970, Australia, Brazili, Finland, Ghana, Japani, Nigeria, na Filipino zilikuwa zimeongezwa kwenye orodha hiyo. Baadhi ya nchi hizi pia zilitokeza mabuku yaliyojalidiwa. Pia miaka ya mapema ya 1970, wamishonari wa Gileadi walifundishwa stadi za uchapaji na kutumwa katika baadhi ya nchi hizi ili kusaidia ndugu wa huko kazi ya uchapaji.
9 Miaka ya 1980, idadi ya nchi ambamo magazeti yalikuwa yakichapwa ilifikia kilele cha 51.a Hayo yalikuja kuwa matumizi mazuri kama nini ya mali ya Bwana-Mkubwa! Huo ulikuwa uthibitisho mkubwa kama nini wa ukuzi wa kazi ya Ufalme! Nao ulikuwa ushuhuda wenye nguvu kama nini wa tegemezo la ukarimu la mamilioni ya Mashahidi wa Yehova mmoja-mmoja ambao ‘walimheshimu Yehova kwa mali yao’! (Mit. 3:9) Hivyo, walijithibitisha wenyewe kuwa wasimamizi-nyumba waaminifu wa yale ambayo Yehova alikuwa amewabarikia katika njia mbalimbali.
-
-
Kutunza Mali za Bwana-MkubwaHuduma ya Ufalme—1998 | Juni
-
-
Mahitaji Mbalimbali ya Kitengenezo
12 Mifumo hii mipya ilibadilisha mahitaji ya kitengenezo ulimwenguni pote ya utendaji wa kuchapa wa Mashahidi wa Yehova. Matbaa za web hufanya kazi haraka sana kuliko matbaa ya kuchapa kama kwa kupiga muhuri, lakini pia ni ghali sana. Mifumo ya kompyuta inayofanya kazi inayohusiana kama vile, uandishi, utafsiri, uchoraji, na upangaji wa chapa, huku ikiwa na uwezo mwingi kuliko ile mifumo ya zamani, ni ghali sana. Upesi ilionekana kwamba halikuwa jambo la kupunguza gharama kuchapa magazeti katika nchi 51 tofauti-tofauti. Kwa sababu hiyo, katika miaka ya 1990 “msimamizi-nyumba mwaminifu” alichunguza mambo tena. Uamuzi ulikuwa nini?
13 Uchunguzi ulionyesha kwamba ‘vitu vyenye thamani’ vilivyochangwa na Mashahidi wa Yehova na rafiki zao vingetumiwa vema zaidi kama kazi ya uchapaji ingeunganishwa. Kwa hiyo idadi ya ofisi za tawi zenye kuchapa ilipunguzwa. Ujerumani imechukua uchapaji wa magazeti na fasihi za nchi nyingi za Ulaya Mashariki na Magharibi, kutia ndani nchi kadhaa ambazo zimekuwa zikifanya uchapaji wao wenyewe. Italia huandaa magazeti na fasihi kwa ajili ya sehemu za Afrika na kusini-mashariki mwa Ulaya, kutia ndani Ugiriki na Albania. Katika Afrika, uchapaji wa magazeti hufanywa Nigeria na Afrika Kusini tu. Kuunganishwa hukohuko kulitokea ulimwenguni pote.
Mambo Fulani ya Kufikiria kwa Uangalifu
14 Kufikia Julai 1998, uchapaji wa magazeti utakomeshwa katika nchi kadhaa za Ulaya kutia na Austria, Denmark, Ufaransa, Ugiriki, Uholanzi, na Uswisi. Kazi ya uchapaji katika Ulaya itashughulikiwa na Finland, Hispania, Italia, Sweden, Uingereza, na Ujerumani. Katika njia hii, gharama zisizo za lazima zingeepukwa na michango ingetumiwa kwa njia bora kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote. Iliamuliwaje kwamba nchi kadhaa ziendelee kuwa sehemu za uchapaji na zipi ziache uchapaji? Kupatana na amri yake ya kutunza kwa hekima mali za Bwana-Mkubwa, “msimamizi-nyumba mwaminifu” alikadiria busara ya kuchapa katika kila sehemu.
15 Sababu kubwa ambayo uchapaji ulikomeshwa katika nchi kadhaa na kuunganishwa katika nyingine ilikuwa kufaa kwa hali. Katika nchi moja uchapaji wa fasihi za nchi nyingine ni jambo lenye kufaa zaidi na ni matumizi bora ya vifaa vilivyo ghali sana. Uchapaji sasa wafanywa mahali ambapo gharama ni za chini, vifaa vyapatikana, na vifaa vya upakizi ni vizuri. Hivyo mali za Bwana-Mkubwa zatumiwa vizuri. Bila shaka, kukomesha uchapaji katika nchi fulani hakumaanishi kwamba kazi ya kuhubiri humo itakoma. Bado kutakuwako wingi wa vichapo vilivyochapwa, na mamia ya maelfu ya Mashahidi wa Yehova katika nchi hizo wataendelea kwa bidii kuambia jirani zao “habari njema ya amani.” (Efe. 2:17) Zaidi ya hilo, huku kurudia kupanga kumetokeza manufaa nyingine.
16 Ili kutaja manufaa moja, matbaa zilizo nyingi za kisasa kutoka Denmark, Ugiriki, Uholanzi, na Uswisi zilipelekwa Nigeria na Filipino. Wafanyakazi walio stadi kutoka nchi za Ulaya walikubali mwaliko wa kwenda pamoja na matbaa hizo ili kuwazoeza wale watakaofanya kazi nazo huko. Kwa sababu hiyo, nchi hizo sasa zinapata magazeti ya hali ya juu ambayo nchi nyingine zimekuwa nayo.
17 Fikiria manufaa nyingine: Gharama ya kuchapa magazeti sasa inachukuliwa na nchi chache ambamo uchapaji bado waendelea. Tokeo ni kwamba, katika nchi ambamo uchapaji umekomeshwa, mali sasa zapatikana kwa makusudi mengine, kama vile kujenga Majumba ya Ufalme na kusaidia kutunza mahitaji ya ndugu zetu katika nchi zilizo maskini zaidi. Hivyo, kutumia kwa uangalifu mali za Bwana-Mkubwa kwamaanisha kwamba maneno ya Paulo kwa Wakorintho yanaweza kutumiwa kwa matokeo zaidi kwa kiwango cha kimataifa: “Sikusudii iwe rahisi kwa wengine, lakini vigumu kwenu; bali kwamba kupitia usawazisho wa ziada yenu sasa hivi ipate kujazia upungufu wao . . . ili usawazisho upate kutukia.”—2 Kor. 8:13, 14.
18 Tokeo la kuunganishwa huku limekuwa kwamba, Mashahidi wa Yehova ulimwenguni wameungana pamoja zaidi kuliko wakati mwingine wowote. Hakuna shida yoyote Mashahidi katika Denmark wakichapiwa magazeti yao Ujerumani, ingawa walikuwa wakichapa yao. Wanashukuru kwa utumishi wa ndugu zao Wajerumani. Je, Mashahidi wa Yehova katika Ujerumani wanaona uchungu kwa sababu michango yao inatumiwa kuandalia Denmark fasihi za Biblia—au Urusi, Ukrainia, na nchi nyingine? La hasha! Wanafurahi kujua kwamba michango ya ndugu zao katika nchi hizi yaweza kutumiwa kwa makusudi mengine ya lazima.
-