Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Utimilifu Wako Unafanya Moyo wa Yehova Ushangilie
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 15
    • 10, 11. (a) Dada yetu mmoja alipambana jinsi gani na majaribu ya utimilifu? (b) Ni jibu gani lenye nguvu ambalo dada huyo alimpa Shetani?

      10 Fikiria mfano wa Dada Valentina Garnovskaya, mmoja kati ya Mashahidi wengi wa Urusi ambao kama Ayubu mwaminifu, walishika utimilifu wao hata ingawa walijaribiwa vikali. Katika mwaka wa 1945, Valentina alipokuwa na umri wa miaka 20 hivi, ndugu mmoja alimhubiria. Ndugu huyo alimtembelea mara mbili ili kuzungumza naye kuhusu Biblia, lakini baada ya hapo Valentina hakumwona tena. Hata hivyo, Valentina alianza kuwahubiria majirani wake. Kwa hiyo, alikamatwa akahukumiwa kifungo cha miaka minane katika kambi moja. Katika mwaka wa 1953, aliachiliwa huru na papo hapo akaanza tena kazi yake ya kuhubiri. Kwa mara nyingine tena alikamatwa na kutupwa gerezani, wakati huo alifungwa miaka kumi. Baada ya kukaa katika kambi moja kwa miaka mingi, alihamishiwa kwenye kambi nyingine. Katika kambi hiyo, kulikuwa na dada fulani ambao walikuwa na nakala moja ya Biblia. Siku moja dada mmoja alimwonyesha Valentina Biblia hiyo. Ulikuwa wakati wenye kusisimua kama nini! Hebu wazia, kabla ya hapo, Valentina hakuwa ameona Biblia nyingine yoyote isipokuwa ile ambayo yule ndugu aliyemhubiria mwaka wa 1945 alikuwa nayo!

      11 Katika mwaka wa 1967, Valentina aliachiliwa huru na mwishowe akabatizwa katika maji ili kuonyesha wakfu wake kwa Yehova. Alitumia uhuru wake kwa kushiriki kwa bidii katika huduma mpaka mwaka wa 1969. Hata hivyo, mwaka huo, alikamatwa tena, na wakati huo alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu gerezani. Lakini, Valentina aliendelea kuhubiri. Kabla ya kifo chake mwaka wa 2001, alikuwa amesaidia watu 44 kujifunza kweli. Alikaa gerezani na katika kambi mbalimbali kwa miaka 21. Alikuwa tayari kupoteza kila kitu, kutia ndani uhuru wake, ili kudumisha utimilifu wake. Mwishoni mwa maisha yake, Valentina alisema hivi: “Sikuwa na mahali pangu pa kuishi. Vitu vyangu vyote vilitoshea katika mfuko mmoja, lakini nilifurahi na kuridhika kwa kuwa nilimtumikia Yehova.” Ni jibu lenye nguvu kama nini ambalo Valentina alimpa Shetani, ambaye alidai kwamba wanadamu hawatabaki washikamanifu kwa Mungu wakijaribiwa! (Ayu. 1:9-11) Tunaweza kuwa na uhakika kwamba aliufanya moyo wa Yehova ushangilie na kwamba Yehova anatazamia kwa hamu sana siku ambayo atamfufua Valentina na wengine wote ambao walikufa wakiwa waaminifu.—Ayu. 14:15.

  • Utimilifu Wako Unafanya Moyo wa Yehova Ushangilie
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 15
    • [Picha katika ukurasa wa 10]

      Valentina alikuwa tayari kudhabihu kila kitu ili kudumisha utimilifu wake

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki