Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Tatizo la Uhalifu Linaweza Kutatuliwa?
    Amkeni!—2008 | Februari
    • Dakt. Stanton E. Samenow anaandika hivi kuhusu njia za sasa za kukabiliana na uhalifu: “Baada ya kufungwa gerezani, [mhalifu] anaweza kujifunza mbinu za kuwa mjanja na mwangalifu zaidi, lakini anaendelea na njia yake ya maisha na kuzidi kufanya uhalifu. Takwimu zinazoonyesha ikiwa mtu amerudia kufanya uhalifu huonekana tu mtu anapokamatwa tena.” Kwa hiyo, magereza yamekuwa kama vyuo vya wahalifu, yakiwasaidia bila kukusudia kuboresha ustadi wao.—Ona sanduku “Je, Magereza Ni Vyuo vya Uhalifu?” kwenye ukurasa wa 7.

  • Je, Tatizo la Uhalifu Linaweza Kutatuliwa?
    Amkeni!—2008 | Februari
    • [Sanduku/ Picha katika ukurasa wa 6, 7]

      “WANAKAMATWA TENA KABLA YA MIAKA MIWILI KWISHA”

      Chini ya kichwa hicho, gazeti The Times la London huko Uingereza, liliripoti kwamba zaidi ya asilimia 70 ya watu nchini Uingereza waliohukumiwa kwa sababu ya kuvunja nyumba na kuiba wanakamatwa tena kabla ya miaka miwili kwisha. Uhalifu mwingi unafanywa na waraibu wa dawa za kulevya ambao wanatafuta pesa za kununua dawa hizo ghali, zinazowadhuru.

      [Sanduku katika ukurasa wa 7]

      “JE, MAGEREZA NI VYUO VYA UHALIFU?”

      “Magereza yamekuwa vyuo vya uhalifu,” aliandika Profesa John Braithwaite katika kichapo chake UCLA Law Review. Dakt. Stanton E. Samenow anasema hivi katika kitabu chake Inside the Criminal Mind: “Wahalifu wengi hujifunza kutokana na mambo yanayowapata,” lakini hawajifunzi kile ambacho jamii inajaribu kuwafundisha. “Huko gerezani,” anaandika, “mtu ana wakati mwingi sana wa kujifunza jinsi ya kuwa mhalifu bora. . . . Kwa kweli wengine wamekuwa wahalifu wenye mafanikio zaidi, wakijitumbukiza kwenye uhalifu lakini wakiwa wajanja ili wasikamatwe.”

      Katika sura nyingine ya kitabu chake, Samenow anasema: “Kifungo hakibadili utu wa mhalifu. Iwe yuko barabarani au gerezani, yeye huwasiliana na wengine, hujifunza mbinu mpya za uhalifu, na kupitisha madokezo fulani kwa wahalifu wengine.” Kijana mmoja mhalifu alisema hivi: “Kufungwa kumenistahilisha kuwa mwalimu wa uhalifu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki