-
Urusi2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
KUUNGANA TENA KWA FURAHA KATIKA IBADA
Ilionekana ni kana kwamba KGB walifanikiwa kusimamisha utendaji wa Mashahidi wa Yehova katika Muungano wa Sovieti, kwa hiyo wakajitayarisha kwa ajili ya shambulizi la mwisho. Mnamo 1960, zaidi ya ndugu 450 walijikuta wamefungwa kwenye kambi moja huko Mordvinia. Ndugu hao walitia ndani wale waliosimamia kazi katika vikundi vyote viwili, yaani, wale waliokuwa wamejitenga na tengenezo na wale ambao hawakuwa wamejitenga. Wapelelezi wa KGB walifikiri kuwa hilo lingewatenganisha kabisa akina ndugu katika tengenezo. Makala yenye dhihaka ilichapishwa katika gazeti la kambi hiyo ya kazi ngumu ikieleza ndugu gani atapigana na nani. Kinyume cha hilo akina ndugu walitumia nafasi hiyo ya kuwa pamoja kuungana.
Iov Andronic anakumbuka hivi: “Ndugu wenye madaraka walimtia moyo kila Shahidi, kutia ndani hata wale waliojitenga na tengenezo kujitahidi kuwa na umoja. Ndugu hao walikazia uangalifu makala ya Kirusi ya Mnara wa Mlinzi la Septemba 1, 1961, yenye kichwa ‘Umoja wa Watu Wote Wenye Nia Nzuri Waahidiwa.’ Makala hiyo ilitoa kanuni na mifano iliyoonyesha jinsi ambavyo Yehova aliwaongoza watu wake nyakati za zamani. Pia, ilizungumzia umuhimu wa kila mmoja kujitahidi kuwa na amani na umoja katika kutaniko la Kikristo. Baada ya kusoma makala hiyo kwa uangalifu, wengi walitambua umuhimu wa umoja wa kitheokrasi na wakafanya mabadiliko yaliyohitajiwa.”
-
-
Urusi2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kwa sababu ya jitihada zangu za kupanda mbegu za kweli kwa wingi, nilianzisha funzo la Biblia pamoja na familia ya injinia mmoja. Muda si muda, yeye na familia yake wakawa Mashahidi wa Yehova na wahubiri wenye bidii. Lakini shirika la KGB lilikuwa likinichunguza na wakati mmoja walipofanya upekuzi walikuta vichapo vya Biblia ndani ya nyumba yangu. Nilihukumiwa kifungo cha miaka 25 na nikapelekwa kwenye kambi ya kazi ngumu katika jiji la Krasnoyarsk, huko Siberia. Nilihamishwa mara nyingi kutoka kambi na magereza mbalimbali. Wakati mmoja, nilihesabu kwamba maishani mwangu nilikuwa nimehamishwa mara 256.
-