-
Kutoka kwa Wasomaji WetuAmkeni!—2002 | Januari 8
-
-
Magereza Asanteni sana kwa mfululizo wenye kichwa “Je, Wafungwa Wanaweza Kurekebishwa?” (Mei 8, 2001) Nilifungwa gerezani kwa miaka 14. Nilipokuwa gerezani nilianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Niliendelea kujifunza baada ya kuachiliwa, na punde baadaye nikabatizwa. Wafungwa wanaweza kurekebishwa wakifuata kanuni za Biblia. Pia, wanapaswa kuwashukuru Mashahidi wanaojitahidi sana kutumia wakati wao kuwasaidia wafungwa. Mimi ninathamini jambo hilo.
R. S., Marekani
Kwa sasa mimi nimefungwa katika gereza ambamo Mashahidi wa Yehova waliruhusiwa kuanzisha masomo yao mazuri. Mfungwa mmoja tayari amebatizwa na wengine wengi hujifunza Biblia. Ni jambo zuri ajabu kumtumikia Yehova popote tulipo!
J. A. M., Marekani
-
-
Kutoka kwa Wasomaji WetuAmkeni!—2002 | Januari 8
-
-
Kwa kuwa nimefungwa gerezani kwa miaka minane iliyopita nimejionea mwenyewe kwamba magereza hayatimizi kusudi lao. Kile kinachofanikiwa ni kazi yenu ya kufundisha Biblia. Ninawashukuru Mashahidi wa Yehova wanaotuonyesha sisi wafungwa upendo. Tulifanya kosa lakini wengine wetu tunajaribu kujirekebisha na kuwa watu bora.
R. J., Marekani
-
-
Kutoka kwa Wasomaji WetuAmkeni!—2002 | Januari 8
-
-
Mfungwa mwenzangu alikuwa mtu wa kwanza kunieleza juu ya Mashahidi wa Yehova. Ninafurahi sana kujua kwamba Mashahidi wa Yehova wana ujasiri wa kutosha kuingia magerezani ili kusaidia watu kama mimi kumjua Yehova kabla ya mwisho. Mashahidi wanapasa kupongezwa kwa upendo wanaoonyesha.
M. N., Marekani
-