Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—2002 | Januari 8
    • Magereza Asanteni sana kwa mfululizo wenye kichwa “Je, Wafungwa Wanaweza Kurekebishwa?” (Mei 8, 2001) Nilifungwa gerezani kwa miaka 14. Nilipokuwa gerezani nilianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Niliendelea kujifunza baada ya kuachiliwa, na punde baadaye nikabatizwa. Wafungwa wanaweza kurekebishwa wakifuata kanuni za Biblia. Pia, wanapaswa kuwashukuru Mashahidi wanaojitahidi sana kutumia wakati wao kuwasaidia wafungwa. Mimi ninathamini jambo hilo.

      R. S., Marekani

      Kwa sasa mimi nimefungwa katika gereza ambamo Mashahidi wa Yehova waliruhusiwa kuanzisha masomo yao mazuri. Mfungwa mmoja tayari amebatizwa na wengine wengi hujifunza Biblia. Ni jambo zuri ajabu kumtumikia Yehova popote tulipo!

      J. A. M., Marekani

  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—2002 | Januari 8
    • Kwa kuwa nimefungwa gerezani kwa miaka minane iliyopita nimejionea mwenyewe kwamba magereza hayatimizi kusudi lao. Kile kinachofanikiwa ni kazi yenu ya kufundisha Biblia. Ninawashukuru Mashahidi wa Yehova wanaotuonyesha sisi wafungwa upendo. Tulifanya kosa lakini wengine wetu tunajaribu kujirekebisha na kuwa watu bora.

      R. J., Marekani

  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—2002 | Januari 8
    • Mfungwa mwenzangu alikuwa mtu wa kwanza kunieleza juu ya Mashahidi wa Yehova. Ninafurahi sana kujua kwamba Mashahidi wa Yehova wana ujasiri wa kutosha kuingia magerezani ili kusaidia watu kama mimi kumjua Yehova kabla ya mwisho. Mashahidi wanapasa kupongezwa kwa upendo wanaoonyesha.

      M. N., Marekani

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki