-
“Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
-
-
1. (a) Biblia hutoa faraja gani kwa wale ambao wameona wapendwa wakipotea njia na kuacha ibada ya kweli? (b) Yehova huwaonaje wakosaji?
“BINTI yangu aliniambia kwamba hakutaka kamwe kuwa mshiriki wa kutaniko la Kikristo,” asema baba mmoja Mkristo. “Kwa muda wa siku nyingi, majuma, na hata miezi mingi baadaye, nilihisi maumivu yenye kusumbua mwilini mwangu. Yalikuwa mabaya zaidi ya kifo.”
-
-
“Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
-
-
Fikiria mwanamke mmoja Mkristo aliyelelewa kulingana na kanuni za Biblia lakini baadaye akaanza kutumia vibaya kileo na madawa ya kulevya. Akikumbuka kipindi hicho chenye kuhuzunisha cha maisha yake, yeye asema: “Nilitaka kuthibitisha kwamba mimi binafsi ningeweza kuboresha maisha yangu. Nilitaka kufanya nilivyotaka, na sikutaka yeyote aniambie nifanye vinginevyo.” Kama mwana mpotevu, mwanamke huyu kijana alitafuta uhuru. Kwa kuhuzunisha, ilibidi aondoshwe kutoka katika kutaniko la Kikristo kwa sababu ya mazoea yake yasiyo ya Kimaandiko.
-
-
“Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
-
-
WALIRUDIWA NA FAHAMU ZAO
Ni nini kilichowasaidia watu fulani ambao wakati mmoja waliondoshwa kutoka katika kutaniko la Kikristo warudie fahamu zao? Maelezo yafuatayo yatuarifu jambo hilo.
“Moyoni mwangu bado nilijua kweli ilipokuwa. Kujifunza Biblia na kuhudhuria mikutano ya Kikristo kwa miaka mingi kulikuwa kumeniathiri sana. Ningewezaje kuendelea kumpuuza Yehova? Hakuwa ameniacha; ni mimi niliyekuwa nimemwacha. Hatimaye, nilikiri jinsi nilivyokuwa mwenye makosa na mwenye shingo ngumu na kwamba Neno la Yehova ni la kweli sikuzote—‘unavuna unalopanda.’”—C.W.
“Mtoto wangu msichana alianza kuongea, na hilo lilinigusa moyo kwa kuwa nilitaka kumfundisha mambo kama vile Yehova ni nani na jinsi ya kusali kwake. Singeweza kulala, na pindi moja usiku sana niliendesha gari hadi kwenye bustani na kulia tu. Nililia, na kusali kwa Yehova kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu. Nilijua tu kwamba nilimhitaji Yehova tena maishani mwangu, nami nilitumaini kwamba angeweza kunisamehe.”—G.H.
“Wakati ambapo habari kuhusu dini ingezuka, ningewaambia watu kwamba kama ningechagua dini iliyofundisha kweli, lazima ningekuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Kisha nilikuwa nikisema kwamba wakati fulani nilikuwa Shahidi, lakini singeweza kuishi kulingana na vile nilivyotarajiwa kuishi, kwa hiyo nikaacha kuwa Shahidi. Nikitambua hilo, mara nyingi nilijihisi mwenye hatia na kukosa furaha. Hatimaye nilikiri, ‘Sina furaha. Ninahitaji kufanya mabadiliko makubwa.’”—C.N.
“Miaka 35 iliyopita mume wangu nami tulitengwa na ushirika. Kisha, mwaka wa 1991, tulifurahi kutembelewa bila kutarajia na wazee wawili waliotufahamisha juu ya uwezekano wa kumrudia Yehova. Miezi sita baadaye, tulifurahi mno kurudishwa. Mume wangu ana umri wa miaka 79, nami 63.”—C.A.
-
-
“Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
-
-
Kwa kielelezo, akiwa na umri wa miaka 17, mwanamume mmoja kijana alikaidi malezi yake ya Kikristo. “Kukosa maadili na matumizi mabaya ya dawa za kulevya yalibatilisha miaka mingi ya mafundisho yaliyotegemea Biblia,” yeye akubali. Punde si punde, mwanamume huyo kijana alijipata gerezani kwa sababu ya unyang’anyi wa kutumia silaha na uuaji kimakusudi. Ingawa baadaye alipata nguvu tena kiroho, alipatwa na mateso makubwa kama nini kwa sababu ya “mfurahio wa muda wa dhambi”!
-
-
“Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
-
-
“Bila mwongozo wa Yehova, nilipatwa na maumivu na huzuni nyingi,” asema mwanamke mmoja kijana ambaye aliacha tengenezo la Mungu kwa muda fulani. “Nilijaribu kujipatanisha na ulimwengu, lakini kwa sababu kwa kweli nilikuwa tofauti na wengine, walinikataa. Nilijihisi kama mtoto aliyepotea ambaye alihitaji baba wa kumwongoza. Ndipo nilipotambua kwamba nilimhitaji Yehova. Sikutaka kamwe kuishi bila kumtegemea.”
-
-
“Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
-
-
Baadhi yao huumizwa sana na mwendo wao mkaidi, na hatimaye wengi wao hurudiwa na fahamu zao. “Sikumsahau Yehova kamwe, hata siku moja,” asema dada mmoja, akikumbuka muda aliokaa nje ya tengenezo la Mungu. “Sikuzote nilisali kwamba kwa njia fulani, siku moja angenikubali niirudie kweli.”—Zaburi 119:176.
-