Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kitabu Kinachotegemeka—Sehemu ya 7
    Amkeni!—2011 | Mei
    • Unabii wa Ufunuo 17:10 unafanana na unabii mwingine unaopatikana katika kitabu cha Danieli. Danieli aliandika kuhusu ‘sanamu kubwa’ ambayo Mfalme Nebukadneza wa Babiloni aliona katika maono aliyopewa na Mungu. (Danieli 2:28, 31-43) Danieli alimfunulia mtawala huyo kwamba sehemu za mwili za sanamu hiyo ziliwakilisha mfuatano wa milki za kisiasa zilizoanza na Babiloni ambayo ndiyo iliyokuwa serikali kuu ya ulimwengu wakati huo. (Misri na Ashuru tayari zilikuwa zimetawala na kutoweka.) Historia sasa inathibitisha mambo yafuatayo:

      Kichwa cha dhahabu kiliwakilisha Milki ya Babiloni.

      Kifua na mikono ya fedha ilifananisha Muungano wa Umedi na Uajemi.

      Tumbo na mapaja ya shaba yaliwakilisha Ugiriki ya kale.

      Miguu ya chuma ilifananisha Milki ya Roma.

      Nyayo zenye mchanganyiko wa chuma na udongo zilifananisha hali ya kisiasa na kijamii isiyo na umoja ambayo ingekuwapo wakati wa utawala wa serikali ya ulimwengu ya Uingereza na Marekani.

      Kulingana na Ufunuo 17:10, serikali kuu ya saba ya ulimwengu ‘lazima idumu kwa muda mfupi.’ Huo ni muda mfupi kadiri gani? Itatokomea namna gani kutoka kwenye tamasha ya ulimwengu? Na nini kitatokea baada yake? Danieli anatupa majibu ya maswali hayo.

      Tumaini Linalotegemeka

      Baada ya kufafanua sanamu ambayo imetajwa, Danieli aliandika hivi: “Jiwe likakatwa [kutoka kwenye mlima] bila kutumia mikono, nalo likaipiga sanamu hiyo juu ya nyayo zake za chuma na za udongo uliofinyangwa, likaziponda.” (Danieli 2:34) Tukio hilo lenye kustaajabisha lilimaanisha nini?

      Danieli aliendelea kusema: “Katika siku za wafalme hao [wa mwisho], Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote [za kidunia], nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo.”b (Danieli 2:44, 45) Zingatia mambo haya muhimu:

      1. Ufalme huo wenye ushindi, unaofananishwa na jiwe kubwa, ‘unasimamishwa’ na Mungu mwenyewe, si kwa “mikono” ya wanadamu. Kwa sababu hiyo, kwa kufaa unaitwa Ufalme wa Mungu.

      2. Ufalme wa Mungu “utazivunja” falme zote za wanadamu, kutia ndani serikali kuu ya saba ya ulimwengu. Kwa sababu gani? Serikali hizo zote zitakataa kuachilia mamlaka na zitampinga Mungu wakati wa vile vita vikuu vya mwisho katika mahali pa mfano panapoitwa Har–Magedoni. Biblia inaeleza waziwazi kwamba vita hivyo vitawahusisha “wafalme wa dunia nzima inayokaliwa.”—Ufunuo 16:13, 14, 16.

      3. Tofauti na serikali za kibinadamu ambazo hazidumu, kutia ndani serikali saba kuu za ulimwengu, Ufalme wa Mungu “hautaharibiwa kamwe.” Pia utaitawala dunia nzima.—Danieli 2:35, 44.

  • Kitabu Kinachotegemeka—Sehemu ya 7
    Amkeni!—2011 | Mei
    • [Mchoro katika ukurasa wa 16]

      (Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

      Babiloni

      Muungano wa Umedi na Uajemi

      Ugiriki

      Roma

      Uingereza na Marekani

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki