-
Yale Anayotabiri Yehova YanatimiaMnara wa Mlinzi—2008 | Januari 1
-
-
Pia, unabii wa Danieli 8:5-8, 21, 22 na 11:3, 4 unatoa habari zenye kustaajabisha kuhusu “mfalme wa Ugiriki” aliyekuwa mkuu isivyo kawaida. Mfalme huyo angeuawa akiwa katika upeo wa mamlaka yake, na ufalme wake ungegawanywa mara nne lakini si kati ya wazao wake. Zaidi ya miaka 200 baada ya unabii huo kuandikwa, Aleksanda Mkuu alithibitika kuwa mfalme huyo mwenye nguvu. Historia ya ulimwengu inatueleza kwamba alikufa kifo cha mapema na kwamba milki yake iligawanywa kati ya majenerali wake wanne, wala si kati ya wazao wake.
Wachambuzi wamedai kwamba unabii huo uliandikwa baada ya tukio hilo. Hata hivyo, chunguza tena masimulizi ya kitabu cha Danieli yaliyotajwa hapo juu. Yanapoonwa kuwa unabii, mambo yanayotajwa humo ni yenye kushangaza. Lakini yanapoonwa kuwa historia inayodaiwa kuwa unabii, je, huoni kwamba masimulizi hayo hayana habari nyingi muhimu? Ikiwa mdanganyifu fulani aliyeishi baada ya Aleksanda alikuwa akijaribu kuwavutia wasomaji kwa masimulizi yanayodaiwa kuwa unabii, kwa nini hakueleza kwamba punde tu baada ya kifo cha Aleksanda, wawili kati ya wana wake wangejaribu kusimamisha ufalme wao lakini wangeuawa? Kwa nini hakutaja kwamba miaka mingi ingepita kabla ya majenerali wote wanne kuimarisha mamlaka yao katika maeneo mbalimbali ya milki ya Aleksanda? Kwa kweli, kwa nini hakutaja majina ya mfalme mkuu na ya majenerali wake wanne?
Madai ya kwamba unabii wa Biblia uliandikwa baada ya matukio ni madai ambayo yameshikiliwa kwa muda mrefu lakini hayajathibitishwa. Madai hayo yametolewa na wale ambao kabla ya kuchunguza uthibitisho wamekata kauli kwamba haiwezekani kutabiri matukio ya wakati ujao. Kwa sababu wanakataa kukubali Biblia kuwa Neno la Mungu, wanalazimika kueleza mambo yote kulingana tu na maoni ya kibinadamu. Hata hivyo, Mungu alitoa kwa hekima habari za kutosha za unabii ili kuthibitisha kwamba yeye ndiye mtungaji wa Biblia.a
-
-
Yale Anayotabiri Yehova YanatimiaMnara wa Mlinzi—2008 | Januari 1
-
-
a Kwa habari zaidi zinazokanusha madai ya kwamba unabii wa Biblia uliandikwa baada ya matukio, ona ukurasa wa 106-111 wa kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.
-