-
Yule Mwanamke Tasa AshangiliaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
5. Katika drama ya mfano iliyoonyeshwa kwenye Wagalatia 4:22-31, ni nani wanaofananishwa na (a) Abrahamu? (b) Sara? (c) Isaka? (d) Hagari? (e) Ishmaeli?
5 Ingawa hivyo, Yehova anawezaje kuwa na wanawake wawili wa mfano—mmoja wa kimbingu na yule mwingine wa kidunia? Je, hali hii inakosa upatano? Hata kidogo. Mtume Paulo anaonyesha kwamba jibu limo katika mfano wa kiunabii uliowekwa na familia ya Abrahamu. (Wagalatia 4:22-31; ona “Familia ya Abrahamu—Mfano wa Kiunabii,” katika ukurasa wa 218.) Sara, yule “mwanamke huru” aliyekuwa mke wa Abrahamu, anafananisha tengenezo la Yehova la viumbe-roho lililo kama mke. Naye Hagari, mjakazi aliyekuwa mke wa pili, au suria, wa Abrahamu anafananisha Yerusalemu la kidunia.
-
-
Yule Mwanamke Tasa AshangiliaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 218, 219]
Familia ya Abrahamu —Mfano wa Kiunabii
Mtume Paulo alieleza kwamba familia ya Abrahamu inatumika kuwa drama ya mfano, mfano wa kiunabii unaoonyesha uhusiano wa Yehova pamoja na tengenezo lake la kimbingu na pamoja na taifa la kidunia la Israeli chini ya agano la Sheria ya Kimusa.—Wagalatia 4:22-31.
Abrahamu, akiwa kichwa cha familia, anawakilisha Yehova Mungu. Hiari ya Abrahamu ya kumtoa Isaka mwanawe mpendwa awe dhabihu inatangulia kuwa kivuli cha hiari ya Yehova ya kumtoa Mwanawe mwenyewe aliye mpendwa sana awe dhabihu ya dhambi za wanadamu.—Mwanzo 22:1-13; Yohana 3:16.
Sara anafananisha “mke” wa kimbingu wa Mungu, yaani tengenezo lake la viumbe-roho. Tengenezo hilo la kimbingu linaelezwa kwa kufaa kuwa mke wa Yehova, kwa sababu linashirikiana na Yehova kindani, linanyenyekea ukichwa wake, na linaonyesha ushirikiano kamili katika utimizaji wa makusudi yake. Mke huyo anaitwa pia “Yerusalemu la juu.” (Wagalatia 4:26) “Mwanamke” huyo huyo anatajwa kwenye Mwanzo 3:15, na ameonyeshwa katika njozi kwenye Ufunuo 12:1-6, 13-17.
Isaka ni ufananisho wa Mbegu ya kiroho ya mwanamke wa Mungu. Kwa msingi, mbegu hiyo ni Yesu Kristo. Hata hivyo, ilikuja pia kuhusisha ndugu watiwa-mafuta wa Kristo, wanaofanywa kuwa wana wa kiroho na kuwa warithi-washirika pamoja na Kristo.—Waroma 8:15-17; Wagalatia 3:16, 29.
Hagari, mke wa pili, au suria, wa Abrahamu alikuwa mtumwa. Kwa kufaa anafananisha Yerusalemu la kidunia, ambapo mfumo wa Sheria ya Kimusa ulitawala, ukiwafunua wote wanaoifuata kuwa watumwa wa dhambi na kifo. Paulo alisema kwamba ‘Hagari anamaanisha Sinai, mlima ulio Arabuni,’ kwa sababu agano la Sheria lilianzishwa huko.—Wagalatia 3:10, 13; 4:25.
Ishmaeli, mwana wa Hagari, anafananisha Wayahudi wa karne ya kwanza, wale wana wa Yerusalemu ambao walikuwa wangali watumwa wa Sheria ya Kimusa. Kama vile Ishmaeli alivyomnyanyasa Isaka, ndivyo Wayahudi hao walivyowanyanyasa Wakristo, waliokuwa wana watiwa-mafuta wa Sara wa mfano, yaani “Yerusalemu la juu.” Na sawa na vile Abrahamu alivyowafukuza Hagari na Ishmaeli, hatimaye Yehova alitupa Yerusalemu na wana wake waasi.—Mathayo 23:37, 38.
-