-
Yesu Ajapo Katika Utukufu wa UfalmeMnara wa Mlinzi—1997 | Mei 15
-
-
Waandamani wa Yesu Waliotukuzwa
9. Je, twapaswa kutarajia Musa na Eliya kuwa pamoja na Yesu katika utimizo wa ono la mgeuko-umbo? Fafanua.
9 Yesu hakuwa peke yake katika ule mgeuko-umbo. Musa na Eliya walionwa pamoja naye. (Mathayo 17:2, 3) Je, walikuwapo kihalisi? La, kwa maana wanaume wote wawili walikuwa wamekufa zamani sana nao walikuwa wamelala usingizi mavumbini wakingojea ufufuo. (Mhubiri 9:5, 10; Waebrania 11:35) Je, wataonekana pamoja na Yesu ajapo katika utukufu wa kimbingu? La, kwa sababu Musa na Eliya waliishi kabla ya tumaini la kimbingu kufunguliwa kwa wanadamu. Watakuwa sehemu ya “ufufuo [wa kidunia] wa waadilifu.” (Matendo 24:15) Hivyo kuonekana kwao katika ono la mgeuko-umbo ni ufananisho. Wa nini?
-
-
Yesu Ajapo Katika Utukufu wa UfalmeMnara wa Mlinzi—1997 | Mei 15
-
-
12. Katika kikao cha mgeuko-umbo, Musa na Eliya ni mifano ya nani?
12 Basi, Musa na Eliya wanawakilisha kimbele nani katika kikao cha mgeuko-umbo? Luka asema kwamba walionekana pamoja na Yesu “wakiwa na utukufu.” (Luka 9:31) Kwa wazi, wanawakilisha kimbele Wakristo ambao wametiwa mafuta kwa roho takatifu wakiwa “warithi-washirika” pamoja na Yesu na ambao hivyo walipokea lile tumaini la ajabu la “kutukuzwa pamoja” naye. (Waroma 8:17) Watiwa-mafuta wanaofufuliwa watakuwa pamoja na Yesu ajapo katika utukufu wa Baba yake ili ‘kumlipa kila mmoja kulingana na mwenendo wake.’—Mathayo 16:27.
Mashahidi Kama Musa na Eliya
13. Ni mambo gani yanayowatia alama Musa na Eliya kuwa mifano ifaayo ya kiunabii ya warithi-washirika watiwa-mafuta wa Yesu wanaotukuzwa pamoja naye?
13 Kuna mambo ya kutokeza yanayowatia alama Musa na Eliya kuwa mifano ifaayo ya kiunabii ya warithi-washirika watiwa-mafuta wa Yesu. Musa na pia Eliya walitumikia wakiwa wasemaji wa Yehova kwa miaka mingi. Wote wawili walikabili hasira ya kisasi ya mtawala fulani. Wakati wa uhitaji, kila mmoja alitegemezwa na familia ya kigeni. Wote wawili walitolea wafalme unabii kwa ujasiri na walisimama imara dhidi ya manabii wasio wa kweli. Musa na pia Eliya waliona udhihirisho mbalimbali wa nguvu za Yehova juu ya Mlima Sinai (ulioitwa pia Horebu). Wote wawili waliweka rasmi waandamizi upande wa mashariki wa Yordani. Na siku za Musa (akiwa pamoja na Yoshua) na pia za Eliya (akiwa pamoja na Elisha) zilikuwa na idadi kubwa kupita zote ya miujiza, kando na ile iliyotukia maishani mwa Yesu.b
14. Watiwa-mafuta wametumikiaje wakiwa msemaji wa Yehova, kama Musa na Eliya?
14 Je, hayo yote hayatukumbushi Israeli wa Mungu? Bila shaka yanatukumbusha. Yesu aliwaambia wafuasi wake waaminifu hivi: “Nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, kuwafundisha kushika mambo yote ambayo mimi nimewaamuru nyinyi. Na, tazameni! mimi nipo pamoja nanyi siku zote hadi umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 28:19, 20) Katika kutii maneno hayo, Wakristo watiwa-mafuta wametumikia wakiwa msemaji wa Yehova tangu Pentekoste 33 W.K. hadi sasa. Kama Musa na Eliya, wamekabili hasira ya kisasi ya watawala na wamewatolea ushahidi. Yesu aliwaambia mitume wake 12 hivi: “Mtaburutwa mbele ya magavana na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushahidi kwao na kwa mataifa.” (Mathayo 10:18) Maneno yake yametimizwa tena na tena katika historia ya kutaniko la Kikristo.—Matendo 25:6, 11, 12, 24-27; 26:3.
15, 16. Kuna ulinganifu gani mbalimbali kati ya watiwa-mafuta kwa upande mmoja na Musa na Eliya kwa upande mwingine katika jambo la (a) kuunga mkono kweli bila hofu? (b) katika kupokea msaada kutoka kwa wasio Waisraeli?
15 Zaidi, kama Musa na Eliya, Wakristo watiwa-mafuta wamekuwa bila hofu katika kuunga mkono kweli dhidi ya mambo ya kidini yasiyo ya kweli. Kumbuka jinsi Paulo alivyomshutumu yule nabii Myahudi asiye wa kweli Bar-Yesu, akafichua kwa busara lakini kwa uthabiti ukosefu wa kweli wa miungu ya Waathene. (Matendo 13:6-12; 17:16, 22-31) Pia, kumbuka kwamba katika nyakati za kisasa mabaki watiwa-mafuta wameifichua kwa ujasiri Jumuiya ya Wakristo na utoaji huo wa ushahidi umeitesa Jumuiya ya Wakristo.—Ufunuo 8:7-12.c
-
-
Yesu Ajapo Katika Utukufu wa UfalmeMnara wa Mlinzi—1997 | Mei 15
-
-
17. Watiwa-mafuta walipatwaje na jambo lifananalo na lile lililompata Eliya juu ya Mlima Horebu?
17 Zaidi, Israeli wa Mungu walipatwa na jambo lifananalo na lile lililompata Eliya juu ya Mlima Horebu.e Kama vile Eliya wakati alipokuwa akikimbia kutoka kwa Malkia Yezebeli, wale mabaki watiwa-mafuta wenye hofu walifikiri kwamba kazi yao ilikuwa imekamilika mwishoni mwa Vita ya Ulimwengu 1. Kisha, sawa na Eliya pia, walimkabili Yehova, aliyekuwa amekuja ili kuhukumu yale matengenezo yaliyodai kuwa “nyumba ya Mungu.” (1 Petro 4:17; Malaki 3:1-3) Ilhali Jumuiya ya Wakristo ilipatikana kuwa imepungukiwa, mabaki watiwa-mafuta walitambuliwa kuwa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” nao wakawekwa rasmi juu ya mali zote za kidunia za Yesu. (Mathayo 24:45-47) Katika Horebu, Eliya alisikia “sauti ndogo, ya utulivu” iliyothibitika kuwa ya Yehova, ikimpa kazi zaidi ya kufanya. Katika kile kipindi cha kimya cha ile miaka ya baada ya vita, watumishi waaminifu wa Yehova watiwa-mafuta walisikia sauti yake kutoka kurasa za Biblia. Wao pia walifahamu kwamba walikuwa na utume wa kutimiza.—1 Wafalme 19:4, 9-18; Ufunuo 11:7-13.
-
-
Yesu Ajapo Katika Utukufu wa UfalmeMnara wa Mlinzi—1997 | Mei 15
-
-
18. Udhihirisho mbalimbali wenye kutokeza wa nguvu za Yehova umeelekezwaje kupitia Israeli wa Mungu?
18 Hatimaye, je, udhihirisho mbalimbali wenye kutokeza wa nguvu za Yehova umeelekezwa kupitia Israeli wa Mungu? Baada ya kifo cha Yesu, mitume walifanya miujiza mingi, lakini hiyo ilikoma hatua kwa hatua. (1 Wakorintho 13:8-13) Siku hizi, hatuoni miujiza kwa maana ya kimwili. Kwa upande mwingine, Yesu aliwaambia wafuasi wake hivi: “Kwa kweli kabisa mimi nawaambia nyinyi, Yeye ambaye hudhihirisha imani katika mimi, huyo pia atafanya kazi ambazo mimi hufanya; naye atafanya kazi kubwa zaidi ya hizi.” (Yohana 14:12) Hilo lilikuwa na utimizo wa kwanza wanafunzi wa Yesu walipokuwa wakihubiri habari njema kotekote katika Milki ya Roma wakati wa karne ya kwanza. (Waroma 10:18) Kazi kubwa hata zaidi zimefanywa leo huku mabaki watiwa-mafuta wakiwa wameongoza kuhubiriwa kwa habari njema “katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya kuwa ushahidi kwa mataifa yote.” (Mathayo 24:14) Tokeo ni nini? Karne ya 20 imeshuhudia kukusanywa kwa idadi kubwa kupita zote ya watumishi waaminifu wa Yehova, waliojiweka wakfu, katika historia. (Ufunuo 5:9, 10; 7:9, 10) Ni uthibitisho mtukufu kama nini wa nguvu za Yehova!—Isaya 60:22.
Ndugu za Yesu Waja Katika Utukufu
19. Ndugu watiwa-mafuta wa Yesu wanaonwa pamoja naye katika utukufu lini?
19 Mabaki ya ndugu watiwa-mafuta wa Yesu wamalizapo mwendo wao wa kidunia, wanatukuzwa pamoja naye. (Waroma 2:6, 7; 1 Wakorintho 15:53; 1 Wathesalonike 4:14, 17) Hivyo wanapata kuwa wafalme na makuhani wasioweza kufa, katika Ufalme wa kimbingu. Wakiwa pamoja na Yesu, ndipo ‘watakapochunga watu kwa fimbo ya chuma hivi kwamba watavunjwa vipande-vipande kama vyombo vya udongo.’ (Ufunuo 2:27; 20:4-6; Zaburi 110:2, 5, 6) Wakiwa pamoja na Yesu, wataketi juu ya viti vya ufalme wakihukumu “yale makabila kumi na mawili ya Israeli.” (Mathayo 19:28) Uumbaji wenye kupiga kite umengojea kwa hamu matukio hayo ambayo ni sehemu ya “kufunuliwa kwa wana wa Mungu.”—Waroma 8:19-21; 2 Wathesalonike 1:6-8.
20. (a) Mgeuko-umbo uliimarisha imani ya Petro kuhusiana na tarajio jipi? (b) Mgeuko-umbo unaimarishaje Wakristo leo?
20 Paulo alisema juu ya kufunuliwa kwa Yesu katika “dhiki kubwa” alipoandika hivi: “Ajapo kutukuzwa kuhusiana na watakatifu wake na kuonwa kwa kustaajabiwa katika siku hiyo kuhusiana na wote wale waliodhihirisha imani.” (Mathayo 24:21; 2 Wathesalonike 1:10) Hilo ni tazamio tukufu kama nini kwa Petro, Yakobo, Yohana, na Wakristo wote watiwa-mafuta kwa roho! Mgeuko-umbo uliimarisha imani ya Petro. Kwa hakika, kusoma juu yao kwaimarisha imani yetu pia na kwatia nguvu uhakika wetu kwamba hivi karibuni Yesu ‘atamlipa kila mmoja kulingana na mwenendo wake.’ Wakristo waaminifu watiwa-mafuta ambao wamesalimika hadi siku hii wanaona uthibitisho wa uhakika wao kwamba watatukuzwa pamoja na Yesu. Imani ya kondoo wengine inaimarishwa katika ujuzi wa kwamba atawaokoa kupitia mwisho wa mfumo huu mwovu wa mambo kuingia katika ulimwengu mpya wenye utukufu. (Ufunuo 7:14) Ni kitia-moyo kilichoje cha kusimama imara hadi mwisho! Na ono hilo laweza kutufundisha mengi zaidi, kama tutakavyoona katika makala ifuatayo.
-