Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ni Nani Atakayeiokoka “Siku ya Yehova”?
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Septemba 15
    • Lakini vipi juu ya kazi ya mwandamizi wa Eliya, nabii Elisha?—1 Wafalme 19:15, 16.

      2. (a) Muujiza wa mwisho wa Eliya ulikuwa nini, nao wa kwanza wa Elisha ulikuwa nini? (b) Kuna ithibati gani ya kwamba Eliya hakuenda mbinguni?

      2 Muujiza wa mwisho uliofanywa na Eliya ulikuwa ule wa kugawanya maji ya Mto Yordani kwa kuyapiga kwa vazi lake rasmi. Hilo liliwawezesha Eliya na Elisha wavuke kupitia ardhi kavu. Walipokuwa wakitembea upande wa mashariki wa huo mto, dhoruba ya upepo ilimchukulia mbali Eliya hadi mahali pengine duniani. (Ona sanduku kwenye ukurasa wa 15 lenye kichwa “Eliya Alipaa Kuingia Mbingu Zipi?”) Vazi rasmi la Eliya liliachwa. Elisha alipolitumia kuupiga Yordani, maji yake yaligawanyika tena, yakimwezesha kurudi kupitia ardhi kavu. Muujiza huo ulionyesha wazi kwamba Elisha alikuwa mwandamizi wa Eliya katika kuendeleza ibada ya kweli katika Israeli.—2 Wafalme 2:6-15.

      Sifa za Kimungu Ni Muhimu

      3. Paulo na Petro walisema nini juu ya kuwapo kwa Yesu na “siku ya Yehova”?

      3 Karne kadhaa baada ya siku za Eliya na Elisha, mtume Paulo na mtume Petro walihusianisha “siku [fulani] ya Yehova” inayokuja pamoja na kuwapo kwa Yesu Kristo na zile ambazo wakati huo zilikuwa “mbingu mpya na dunia mpya” za wakati ujao. (2 Wathesalonike 2:1, 2; 2 Petro 3:10-13) Ili kuokoka siku kuu ya Yehova—Mungu aangamizapo maadui wake na kuokoa watu wake—lazima tumtafute Yehova na kuonyesha usikivu na uadilifu. (Sefania 2:1-3) Lakini sifa nyingine za ziada zaonekana tufikiriapo kwa uangalifu matukio yanayomhusisha nabii Elisha.

      4. Bidii ina fungu gani katika utumishi wa Yehova?

      4 Bidii kwa ajili ya utumishi wa Mungu ni muhimu ikiwa tutaokoka “siku ya Yehova.” Eliya na Elisha walikuwa wenye bidii katika utumishi wa Yehova. Wakiwa na bidii hiyohiyo, leo baki la Wakristo watiwa-mafuta humtolea Yehova utumishi mtakatifu na huongoza katika kuhubiri habari njema.a Tangu katikati ya miaka ya 1930, wamewatia moyo wote wanaokubali ujumbe wa Ufalme na kutumainia kuishi milele duniani wajiweke wakfu kwa Yehova na kubatizwa. (Marko 8:34; 1 Petro 3:21) Mamilioni ya watu wameitikia kwa mwelekeo mzuri kitia-moyo hicho. Wakati mmoja walikuwa katika giza la kiroho na wafu katika dhambi, lakini sasa wamejifunza kweli ya Mungu, wamekubali lile tumaini la uhai wa milele kwenye paradiso ya kidunia, nao wamekuwa wana bidii katika utumishi wa Yehova. (Zaburi 37:29; Ufunuo 21:3-5) Kwa bidii, kushirikiana, ukaribishaji-wageni, na matendo yao mengine yaliyo mema, wao huburudisha sana ndugu wa Kiroho wa Kristo walio duniani bado.—Mathayo 25:31-46.

      5. Kwa nini ni jambo la maana sana kufanyia “ndugu” za Yesu mambo mema, nasi tuna kielelezo gani cha siku ya Elisha?

      5 Wawafanyiao “ndugu” za Yesu mambo mema kwa sababu hao watiwa-mafuta ni wafuasi wake, wana tumaini la kuokoka “siku ya Yehova.” Mume na mke katika kijiji cha Shunemu walibarikiwa sana kwa kuwa wenye fadhili kwa Elisha na hadimu wake na kwa kuwakaribisha. Mume na mke hao hawakuwa na mwana, naye mume alikuwa mzee. Lakini Elisha alimwahidi huyo mwanamke Mshunami kwamba angezaa mwana, na hilo kwa hakika lilitukia. Mwana huyo wa pekee alipokufa miaka kadhaa baadaye, Elisha alienda Shunemu na kumfufua. (2 Wafalme 4:8-17, 32-37) Ni thawabu nyingi kama nini kwa kumkaribisha Elisha!

      6, 7. Naamani aliweka kielelezo gani, na hilo laathirije kuokoka “siku ya Yehova”?

      6 Unyenyekevu unahitajiwa ili kukubali mwelekezo wenye kutegemea Biblia kutoka kwa “ndugu” za Kristo kukiwa na tumaini la kuokoka siku ya Yehova. Naamani, mkuu wa jeshi Msiria, alilazimika kuonyesha unyenyekevu ili kufuata dokezo la msichana Mwisraeli aliyetekwa na kutafuta ponyo kwa kwenda Israeli kumtafuta Elisha. Badala ya kutoka nyumbani kwake ili amlaki Naamani, Elisha alimtumia ujumbe huu: “Enenda ukaoge katika Yordani mara saba, na nyama ya mwili wako itakurudia, nawe utakuwa safi.” (2 Wafalme 5:10) Kujionea fahari kwa Naamani kulikosewa, naye akakasirika, lakini baada ya kwenda kwa unyenyekevu na kujichovya Yordani mara saba, “nyama ya mwili wake ikarudi ikawa kama nyama ya mwili wa mtoto mchanga, akawa safi.” (2 Wafalme 5:14) Kabla ya kurudi nyumbani, Naamani alifunga safari ndefu kurudi Samaria ili kumshukuru nabii wa Yehova. Akiwa ameazimia kutofaidika kimwili kutokana na nguvu zenye kupewa na Mungu, Elisha alitoka ili amlaki Naamani, lakini hakukubali zawadi zozote. Naamani alimwambia Elisha hivi kwa unyenyekevu: “Mtumwa wako hatatoa tena sadaka ya kuteketezwa wala dhabihu kwa miungu mingine, ila kwa BWANA [“Yehova,” NW].”—2 Wafalme 5:17.

      7 Kwa kufuata kwa unyenyekevu shauri la Kimaandiko la watiwa-mafuta, mamilioni ya watu wanabarikiwa sana leo. Isitoshe, kwa kudhihirisha imani katika dhabihu ya fidia ya Yesu, watu hao wenye moyo wa haki wamesafishwa kiroho. Sasa wanaonea shangwe pendeleo la kuwa marafiki wa Yehova Mungu na Yesu Kristo. (Zaburi 15:1, 2; Luka 16:9) Na ujitoaji wao kwa Mungu na kwa utumishi wake utathawabishwa kwa kuhifadhiwa kwao wasipatwe na uharibifu wa milele ukaribiao kuwapata wakosaji wenye kiburi, wasiotubu, katika “siku ya Yehova” inayokaribia kwa kasi.—Luka 13:24; 1 Yohana 1:7.

      “Aliye Upande Wangu Ni Nani?”

      8. (a) Watakaookoka “siku ya Yehova” wana mtazamo gani kuelekea kufanya mapenzi ya kimungu? (b) Yehu alipewa utume gani? (c) Yezebeli alipasa kupatwa na nini?

      8 Wanaotumainia kuokoka “siku ya Yehova” lazima pia waamue kufanya mapenzi ya kimungu. Eliya alitabiri kwa ujasiri kuharibiwa kwa familia ya Mfalme Ahabu yenye kuua kimakusudi na kuabudu Baali. (1 Wafalme 21:17-26) Hata hivyo, kabla ya ufishaji huo kufanywa, ilikuwa lazima Elisha, mwandamizi wa Eliya, akamilishe kazi fulani ambayo haikuwa imemalizika. (1 Wafalme 19:15-17) Wakati wa Yehova ulipowadia, Elisha alimwagiza hadimu aende na kumtia mafuta Yehu, mkuu wa jeshi, awe mfalme mpya wa Israeli. Baada ya kuyamimina mafuta juu ya kichwa cha Yehu, huyo hadimu alimwambia hivi: “BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nimekutia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa BWANA, yaani, juu ya Israeli. Nawe utawapiga nyumba ya Ahabu, bwana wako, ili nijilipize kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii, na damu ya watumishi wote wa BWANA, mkononi mwa Yezebeli. Kwa maana nyumba yote ya Ahabu wataangamia.” Malkia Yezebeli mwovu angetupwa kwa mbwa na asipate kuzikwa kwa heshima.—2 Wafalme 9:1-10.

  • Ni Nani Atakayeiokoka “Siku ya Yehova”?
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Septemba 15
    • Kutumikia kwa Bidii ya Elisha

      16, 17. (a) Twajuaje kwamba Elisha alikuwa mwenye bidii hadi mwisho wa uhai wake? (b) Twapaswa kufanya nini na mishale ya kweli?

      16 Mpaka “siku ya Yehova” ikomeshapo mfumo wote mwovu wa mambo wa Shetani, watumishi wa Mungu watakuwa na ujasiri na wenye bidii kama Elisha. Mbali na kazi yake akiwa hadimu wa Eliya, Elisha alitumikia peke yake akiwa nabii wa Yehova kwa miaka zaidi ya 50! Naye Elisha alikuwa mwenye bidii hadi mwisho wa maisha yake marefu. Kabla tu ya kifo chake, alitembelewa na mjukuu wa Yehu, Mfalme Yehoashi. Elisha alimwambia apige mshale nje ya dirisha. Huo mshale ukaenda mbio hadi kwenye shabaha yake, naye Elisha akasema kwa mkazo hivi: “Mshale wa BWANA wa kushinda, naam, mshale wa kushinda Shamu, kwa maana utawapiga Washami katika Afeki hata utakapowaangamiza.” Kisha Elisha alipomwomba, Yehoashi alipiga ardhi kwa mishale yake. Lakini alifanya hilo bila bidii, akipiga mara tatu tu. Ndipo Elisha akasema kwamba, kwa sababu hiyo, Yehoashi angepewa ushindi mara tatu tu dhidi ya Shamu, na ndivyo ilivyotokea. (2 Wafalme 13:14-19, 25) Mfalme Yehoashi hakuwaangusha Washami kikamili, ‘hata kuwaangamiza.’

      17 Ingawa hivyo, wakiwa na bidii kama ya Elisha, baki la watiwa-mafuta huendeleza pigano dhidi ya ibada isiyo ya kweli. Waandamani wao wenye matumaini ya kidunia wanafanya vivyo hivyo. Isitoshe, wote wanaotumaini kuokoka “siku ya Yehova” hufanya vema kukumbuka maneno ya Elisha mwenye bidii juu ya kuipiga ardhi. Acheni tuchukue mishale ya kweli na kuipiga kwa bidii—tena na tena—ndiyo, hadi Yehova asemapo kazi tufanyayo na mishale hiyo imekamilika.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki